STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, September 26, 2013

'Ulimbukeni unawasumbua wana hip hop'


Ile Ile
MSANII anayezidi kuja juu nchini katika muziki wa Hip Hop, Maishani Ndee 'Ile Ile' amedai ulimbukeni na kutaka kuiga kila kitu toka Marekani ndiko kunakowasumbua baadhi ya wasanii wa miondoko hiyo na kudiriki kujihusisha na matukio ya kibabe.
Ile Ile alisema siyo kweli kama mtu kuwa msanii wa hip hop ni lazima awe mtemi, mfanya fujo na anayejihusisha na matumizi ya pombe au dawa za kulevya isipokuwa wanaofanya hivyo wanasumbuliwa na kasumba ya kuiga mambo tu.
"Binafsi sikubaliani na mambo yanayofanywa na baadhi ya wasanii wa miondoko ya Hip Hop ya kufanya fujo, kujitia wababe na matukio mengine ya ovyo, naamini wanaofanya hivyo wanasumbuliwa na ulimbukeni wa kuiga kila jambo bila kujali kama ni zuri au la ama linaloendana na utamaduni wa Kitanzania," alisema.
Ile Ile anayetamba na nyimbo kama 'Ile Ile', 'Bora Liende' na 'Wazazi' aliouachia hivi karibuni, alisema mila na tamaduni za hip hop ni amani na upendo na kukomboa wengine sna kuhoji ni vipi sasa wanahip hop kupenda kuwanyanyasa wengine.
Alisema ni lazima wasanii wa miondoko hiyo wajaribu kuepuka mambo hayo ambayo alidai yanachangia kuufanya muziki huo kuchukuliwa kama wa wahuni ilihali karibu dunia nzima inakombolewa na harakati za wanahip hop.
Msanii huyo alisema pia japo kila mtu ana uhuru wake wa kutumia kitu chochote, bado wasanii wanapaswa kuepuka matumizi ya ulevi na dawa za kulevya kwani ndizo zinazochangia wengi wao kuwa wakorofi na kuharibu sifa za hip hop.

No comments:

Post a Comment