STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, September 26, 2013

Vodacom yazipiga tafu Shule 12 vifaa vya michezo






KAMPUNI ya VODACOM Tanzania imetoa vifaa vya michezo vyenye thamani ya shilingi milioni 11kwa shule 12 za Sekondari katika mkoa wa Dar es Salaam ikiwa na lengo la kukuza mchezo wa soka kuanzia ngazi za chini.
Msaada huo umekabidhiwa na Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa VODACOM Tanzania Kelvin Twissa kwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mkandara leo jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waanahabari Twissa alisema msaada huo ni mwendelezo wa kampuni yao katika kuhakikisha kuwa michezo inakuwa nchini kuanzia ngazi ya chini ambapo wanatarajia kuendelea na mikoa mingine.
Twissa alisema VODACOM pamoja na ukweli kuwa imekuwa ikisaidia sekta mbalimbali ila michezo ni sehemu kubwa ya ufadhili wao wakiamini kuwa ni sehemu ambayo inahusisha jamii kubwa.
“Mh. Waziri napenda kukuambia baada ya majadiliano yetu ya muda tumeweza kutoa msaada huu kwa kuanza ambapo zipo jezi pea 12 na mipira 40 jambo ambalo litaweza kuleta tija kwa sasa,” alisema.
Kwa upande Waziri Mkandara alisema wizara yake imefarijika sana kwa kupata msaada huo kwani ni moja ya malengo yao ya kukuza michezo kwa kushirikiana na wadau wengine.
Alisema lengo lao ni kuhakikisha kuwa michezo inachezwa kila wakati katika maeneo yote ya nchi hasa kwa kuanzia ngazi ya shule za msingi na sekondari ili kuwa na mwelekeo mzuri wa kimichezo.
Dk. Mkandara alisema mashindano hayo ya majaribio yatahusisha Wilaya tatu za mkoa wa Dar es Salaam kwa kila Wilaya kutoa shule nne za sekondari ambao michezo miwili ya mpira wa pete na mpira wa miguu.
Waziri alisema michezo ni ajira, afya na pia inajenga akili hivyo ni vyema kwa kuanzia ngazi ya chini ili iweze kuwaathiri vijana wakiwa wadogo.
Aidha waziri alitoa rai kwa wadau mbalimbali na taasisi kujitokeza kusaidia michezo mbalimbali kwani hiyo ndiyo njia sahihi ya kufikia malengo ya kukuza michezo hapa nchini.

No comments:

Post a Comment