STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 12, 2013

Filama ya Dasmila karibuni kutoka hadharani

FILAMU  mpya ya Dasmila inatarajia kuingia sokoni mwishoni mwa mwezi huu. Akizungumza jijini Dar, Mkurugenzi wa  DJ Marketing & Promotion ambao ndio wasambazaji wa kazi hiyo, Haulle Daniel amesema kazi hiyo ime kamilika kwa asilimia zote hivyo wapenzi wa filamu wakae mkao wa kula kwani imewashirikisha wasanii wengi akiwemo Shamsa Frod,Jack Pentzel, Elias Mkali, Shaban Dicosta na wasanii wengine wanaotamba katika anga za filamu nchini. Filamu hiyo ya mapenzi ambayo kuna mambo mbalimbali ya kuelimisha jamii ya kitanzania ambapo Dasmila aliyeuawa kipindi cha nyuma kidogo, arudi tena kama mzimu, na mengi yanatokea. Fuatilia.. Familia, vichekesho na vimbwanga, mapenzi, kukosa uaminifu, visa na mikasa kibao  ambayo yatapatikana katika filamu hiyo, ambayo imetengenezwa kwa ubora wa ali ya juu na itakayokuwa ikisambazwa na kampuni ya kizalendo ya DJ Marketing ya jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment