STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 12, 2013

Golden Bush, Pugu Veterani kuvaana kesho Kinesi

Ticotico (kushoto) katika moja ya mechi zao za maveterani

WAKALI wa soka la maveterani jijini Dar es Salaam, Golden Bush Veterani kesho asubuhi inatarajiwa kuvaana na Pugu Veterani katika pambano la kukata na shoka la kirafiki litakalochezwa kwenye uwanja wa Kinesi, Ubungo jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa ya uongozi wa Golden Bush inayoundwa na wakali za zamani wa Simba na Yanga, mechi hiyo ni ya kumaliza mzizi wa fitina baada ya tambo za muda mrefu, huku wakali hao wa soka la jiji wakiwatisha Pugu kwamba wajiandae kupokea kipigo kikali hiyo kesho.
Taarifa ya Golden Bush kupitia Msemaji na mlezi wa klabu hiyo, Onesmo Waziri 'Ticotico' inasomeka hivi:

Wadau,
 
Kutokana na vipigo vya mfululizo kutoka kwa wapinzani wetu wakiwepo Pugu Veterans, na tambo nyingi kutoka kwa wapinzani wetu hapa jijini, Golden bush tumelazimika kuomba mechi ya kirafiki ya marudiano na Pugu Veterans, game itapigwa uwanja wa Kinesi maarufu kama St James Park siku ya jumapili asubuhi.  Kwakutambua umuhimu ya game hii, uongozi wetu umeitisha kikao cha dharula kesho baada ya mazoezi asubuhi ili kuweka mikakati kabambe ya kurudisha heshima ya timu yetu ambayo mpaka sasa inatambulika kama mabingwa wa jiji la Dar es Salaam. Timu yetu imekamilika kabisa hakuna majeruhi hakuna mgonjwa hakuna mgogoro, uwanja uko sawa kamati ya ufundi inamaalizia kazi yake kwa kushirikiana na Walimu wetu. Tumejiwekea lengo la kufunga magoli mengi iwezekanavyo ili kuvunja rekodi ya kufunga magoli.
 
Aidha ningependa kutoa taarifa kwamba timu yetu imeimarika zaidi  mara baada ya Juma Kaseja, Said Swedi ,Mwarami Mohamed na Shadrack Nsajigwa  kurejea kwenye timu yetu.  karibuni mje muone soka la hali ya juu sana huku likihanikizwa na ufundi wa vijana wa zamani chini ya kocha wetu Madaraka Selemani “Mzee wa kiminyio”
 
Baada ya game ya jumapili, timu itakuwa kwenye maandalizi ya mwisho kabisa kwenda kucheza mechi za kirafiki visiwani Zanzibar.
 
Asanteni kwa kunisikiliza.
Onesmo Waziri “Ticotico” Mchezaji Mwandamizi

No comments:

Post a Comment