STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, October 21, 2013

Gaucho akiri 'gemu' kumkataa lakini akwepa mzigo wa lawama

Abdulhalim Humud 'Gaucho'
KIUNGO Mshambuliaji wa Simba, Abdulhalim Humud 'Gaucho' amekiri kwamba hakuwa katika kiwango kizuri katika pambano lao la juzi dhidi ya wapinzani wao wa jadi Yanga, akidai 'gemu' lilimkataa, lakini amesema hadhani kama anapaswa kubebeshwa mzigo wa lawama kwa namna timu ilipocheza katika kipindi cha kwanza.
Kocha Mkuu wa Simba, Abdallah KIbadeni 'King' alikaririwa akimtupia lawama kiungo huyo kwa matoikeo ya 3-0 iliyopatya timu yake katika kipindi cha kwanza kabla ya kumtoa na nafasi yake kuchukuliwa na Said Ndemla na Simba kurejesha mabao yote matatu na kulazimisha sare ya mabao 3-3.
Akizungumza na MICHARAZO asubuhi hii Gaucho, alisema anamheshimu kocha wake na anaheshima kauli yake kutokana na Simba kucheza ovyo kipindi cha kwanza, lakini alisema kwake anaamini 'gemu' lilimkataa japo linaloweza kumtopkea mchezaji yeyote duniani.
Gaucho alisema anaamini kocha alimpanga kwa uwezo alionao na alioonyesha katika mechi kadhaa za nyuma, ila bahati mbaya gemu lilimkataa na hivyo kutocheza vyema, japo alisema hapaswi kulaumiwa pekee yake kwani karibu timu nzima ilishindwa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.
"Sijamsikia kocha akiyasema unayoniambia ila kama amenitupia lawama, sidhani kama ni sawa kwa sababu timu nzima katika kipindi cha kwanza hatukucheza vyema na kutimiza wajibu wetu, ila namheshimu kauli yake, japo lazima nikiri kwamba nilijiandaa sana kwa mchezo huo ila 'gemu' lilinikataa," alisema Gaucho.
Mchezaji huyo alirejea Simba akitokea Azam msimu uliopita, alisema kama mchezaji anajisikia vibaya kunyooshewa vidole kwa sababu inaweza kutafisriwa vibaya na mashabiki ilihali amekuwa akijitolea kwa uwezo wake kuhakikisha Simba inafanya vyema.
Kibadeni alionyesha kukerwa na baadhi ya wachezaji akiwamo Gaucho kwa jinsi walivyocheza katika kipindi cha kwanza na Simba kulala mabao 3-0 kabla ya kufanya mabadiliko na kusaidia kurejea mabao yote matatu kupitia kwa Betram Mombeki, Joseph Owino na Kaze Gilbert na kuifanya timu hiyo ipumue katika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 19.
Timu hiyo inatarajiwa kushuka dimbani keshokutwa kuvaana na Coastal Union ya Tanga katika mfululizo wa ligi hiyo iliyopo raundi ya 10 kwa sasa. Mechi hiyo itachezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga.

No comments:

Post a Comment