STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, October 21, 2013

Simba, Yanga waingiza Mil. 500

Wachezaji wa Simba na Yanga walipokuwa wakiumana jana
Na Boniface Wambura
PAMBANO la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jana baina ya watani wa jadi Simba na Yanga lililochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa sare ya mabao 3-3 limeingiza jumla ya Sh. Milioni 500.7.
Mashabiki 57,422 ndiyo waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo namba 63 kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000 na sh. 30,000.
Ni tiketi 131 tu ndizo hazikuuzwa ambazo ni 90 za VIP A, 40 za VIP B na moja ya VIP C. Tiketi zilizochapwa kwa ajili ya mechi hiyo ni 57,558 ambayo ndiyo idadi ya viti vilivyopo kwenye uwanja huo. Kila klabu imepata mgawo wa sh. 123,025,564.32 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 76,382,084.75.
Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 62,555,371.69, tiketi sh. 7,309,104, gharama za mechi sh. 37,533,223.01, Kamati ya Ligi sh. 37,533,223.01, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 18,766,611.51 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 14,596,253.39.

No comments:

Post a Comment