STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, October 31, 2013

Hii ndiyo ratiba ya 8 Bora Capital One


MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya England Manchester United imepangiwa kucheza ugenini dhidi ya Stoke City katika pambano lake la Robo Fainali ya Kombe la Ligi (Capital One) baada ya FA kutangaza ratiba ya Nane Bora.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo ilivyo ni kwamba Manchester City nayo itacheza ugenini dhidi ya timu ya Daraja la Kwanza Leichester City, huku Tottenham Hotspur watakuwa nyumbani kuvaana na 'Wagonga Nyundo wa London' West Ham United.
Chelsea wenyewe wamepangiwa kuumana na mshindi wa mechi ya mwisho ya hatua ya nne ya michuano hiyo kati ya Sunderland na Southampton.

No comments:

Post a Comment