STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, October 31, 2013

Tottenham, Manchester City zaifuata Chelsea, Man Utd Capital One League

Manchester City wakipongezana

Wachezaji wa Spurs wakipongeza baada ya kufuzu Roibo Fainali ya Capital One L:eague jana
TIMU za Tottenham Hotspur na Manchester City usiku wa kuamkia leo nazo zimefanikiwa kutinga hatua ya Robo Fainbaliu ya Kombe la League (Capital One) baada ya kupata ushindi kwa mbinde dhidi ya wapinzani wao kwenye mechi za raundi ya nne ya michuano hiyo.
Spurs ililazimika kusubiri mikwaju ya penati kuwavusha hatua hiyo mbele ya Hull City baada ya kumaliza dakika 120 zikiwa nguvu sawa ya kufungana mabao 2-2.
Ikicheza nyumba Spurs ilitangulia kupata bao la kuongoza dakika ya 16 kupitia kwa Gylfi Sigurdsson na kudumu hadi kipindi cha kwanza kinamalizika.
Kipindi cha pili kilianza kwa kipa wa Spurs, 'Babu' Brad Friedel kujifunga bao dakika ya 53 na kuisafanya Hull kupumua na kumaliza dakika 90 zikiwa bao 1-1 na katika dakika za 30 za nyongeza, McShane aliiandikia wageni bao dakika ya 99 kabla ya wenyeji kuchomoa dakika ya 108 baada ya Harry Kane kufunga bao na kuingia kwenye matuta ya penati.
Katika hatua hiyo Spurs ilifanikiwa kutumbukiza penati 8 na Hull City 7 na kufanya Spurs kuungana na vigogo vya Manchester United, Chelsea na Manchester City iliyopata ushindi wa mbinde ugenini dhidi ya  Newcastle United kucheza hatua ya Robo Fainali.
Man City iliishinda Newcastle 2-0 katika muda wa nyongeza baada ya awali kumaliza dakika 90 zikiwa nguvu sawa kwa kutofunagana.
Katika muda huo wa nyongeza mabingwa hao wa zamani wa Ligi Kuu ya England walipata mabao yao dakikka za 99 na 105 kupitia kwa Negredo na Eden Dzeko.
Timu nyingine zilizofuzu hatua hiyo ya Robo Fainali ya Capital One ni Stoke City, West Ham United na Leicester City, huku timu ya mwisho kumalizia nafasi moja iliyosalia itasubiri matokeo ya wiki ijayo kati ya Sunderland dhidi ya Southampton itakayochezwa Novemba 6.

No comments:

Post a Comment