STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, October 31, 2013

Simba yavutwa mkia jioni, mashabiki wang'oa viti FFU yawafurumusha kwa mabomu ya machozi

Kagera walioinyima raha Simba leo Taifa
BAO la mkwaju wa penati lililofungwa dakika za majeruhi na beki Salum Kanoni limeisaidia Kagera Sugar kunusurika kipigo toka kwa Simba baada ya kulazimisha sare ya 1-1 katika pambano la Ligi Kuu Tanzania Bara.
Mwamuzi Mohammed Theophile wa Morogoro alitoa penati hiyo baada ya mabeki wa Simba kumuangusha Jumanne Daudi katika lango lao na kusababisha vurugu kubwa kutoka kwa mashabiki wa Simba ambao wanadaiwa walikuwa waking'oa viti na kulazimisha FFU kuvurumusha mabomu ya machozi.
Kabla ya penati, Simba ilionekana kuelekea kuibuka washindi katika pambano hilo lililokuwa kali kwa bao la dakika za majeruhi ya kipindi cha kwanza lililofungwa na Mrundi Amissi Tambwe.
Tambwe alifunga bao hilo kwa shuti kali na kuifanya Simba iende mapumziko ikiwa mbele kwa bao 1-0 ambalo liliendelea mpaka ilipofika dakika nne za nyongeza wakati Kagera waliposhambulia lango na wekundu hao wa msimbazi na kumchezea vibaya Daud.
Kitendo cha kutolewa kwa penati hiyo ilionekana kuwakera benchi nzima la Simba pamoja na mashabiki wao, lakini mwamuzi alisimamia msimamo wake na Kanoni aliyewahi kuichezea Simba kufunga bao hilo na kufanya mashabiki wa Msimbazi kuanza kung'oa viti kwa hasira.
Kwa matokeo hayo ya sare hiyo, Simba imeshindwa kurejea kileleni kwa kufikisha pointi 21 inayowafanya wasalie katika nafasi yao ya nne waliokuwa wakiishikilia nyuma ya Yanga ambayo kesho itashuka kwenye uwanja huo kuvaana na JKT Ruvu.
Azam na Mbeya City zinaendelea kubaki kileleni zikiwa na pointi 23 na Yanga wakifuatia nafasi ya tatu wakiwa na pointi 22 na kama kesho watashinda wanaweza kukaa kileleni mpaka Jumamosi wakati Azam itakaposhuka dimbani kuvaana na Ruvu Shooting.

No comments:

Post a Comment