STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, October 31, 2013

Mtanzania kuwania ubingwa wa Dunia wa WBC

Bondia Omer Kimweri
BONDIA Mtanzania anayefanya shughuli zake nchini Australia, Omari Kimweri 'Lion Boy' anatarajiwa kuwa Mtanzania wa kwanza kupanda ulingoni kuwania taji la Dunia la WBC katika pambano litakalofanyika Novemba 30.
Kimweri atapanda ulingoni katika pambano la uzito wa Minimum (kilo 47.5) nchini China kupigana na bingwa mtetezi wa taji hilo duniani, Mchina Xiong Zhao Zhong.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotumwa kwa MICHARAZO, Kimweri amepata nafasi ya kupigana na Zhong kutokana na rekodi nzuri aliyonayo katika mchezo huo akiwa amepanda ulingoni mara 16 na kushinda michezo 13.
Kati ya michezo hiyo Mtanzania huyo amepoteza michezo mitatu tu, wakati mpinzani wake amecheza michezo 26 na kushinda 21 na kupigwa michezo minne na mmoja kuambulia sare hali inayoonyesha pambano hilo litakuwa kali.
"Kura zilimuangukia Kimweri baada ya kutakiwa bondia kutoka Afrika mwenye rekodi nzuri kupambana na bingwa huyo wa dunia wa WBC Minimum Weight, hivyo Kimweri anakuwa Mtanzania wa kwanza kuwania taji hilo," taarifa hiyo ilisomeka hivyo.
Mara ya mwisho kwa Mtanzania huyo kupanda ulingoni ilikuwa Julai 25 mwaka huu ambapo aliibuka na ushindi wa TKO ya raundi ya kwanza.
Kimweri yupo kwenye mazoezi makali akifanyishwa akisaidiwa na bondia bingwa wa Lightfly kutoka Ufilipino, Randy Petalcoria.

No comments:

Post a Comment