STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, December 12, 2013

BARAZA lafungia shindano la Miss Utalii Tanzania, kisa...!

BARAZA  la Sanaa la Taifa (BASATA) limeyafungia mashindano ya urembo ya Utalii 'Miss Tourism Tanzania' kutokana na kukiuka taratibu na maagizo ya baraza hilo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Afisa Habari Mkuu wa baraza hilo, Agness Kimwaga inaelezwa kuwa Miss Utalii imefungiwa kwa sababu kuu mbili;
taarifa hiyo ya BASATA inasomeka kama ifuatavyo;

Baraza la sanaa Taifa limefungia mashindano hayo kutokana na sababu kuu mbili,kwamza mashindano Miss Tourism Tanzania 2013 kushindwa kufanya tathmini ya mashindano ya miss Tourism 2012/2013 kwa muda uliokubalika baada ya maonyesho hayo kufanyika,na sababu nyingine kwamba Miss Tourism Tanzania kukiuka masharti,kanuni,miongozo na taratibu za uendesheaji wa mashindano ya urembo kama zilivyowekwa na serikali kupitia Baraza la Sanaa la Taifa kwa hiyo hizo ndo sababu zilizofanya sisi kulifungia shindano hili kwa muda usiojulikana"
"Tukiwa na ushahidi uliokamilika kutoka kwa warembo wenyewe waliohusika hatuwezi kufungia kitu pasipo ushahidi,kumbuka mashindano haya yanapokuwa yanaendelea serikali hatukai kwenye zile kambi kwa muda wote wanaokaa kwa kuwa mara nyingi tunapokwenda kutembelea warembo wakiwa kwenye zile kambi tunawaambia popote panapokua na tatizo kunakiukwa taratibu tunawapa taratibu tunazotaka zifuatwe zinapokiukwa wao watupe taarifa,tusipopata taarifa sisi hatuwezi kumfungia mtu pasipo kuwa na taarifa tumekua na taarifa za uhakika toka kwa warembo wenyewe ndo maana tumechukua hatua".
"Tunasema kwamba tunapoendesha shughuli yoyote ya sanaa usifanye vitu ambavyo vinaweza kumdharirisha mtazamaji au mhusika anaefanya kitu kile kwa hiyo kuna vitu ukifanya vinaweza kumdharirisha mtu kwa njia moja au nyingine umekiuka kanuni na taratibu kumnyanyasa mfano kijinsia,kwanza kabla ya kukufungia tunakupa pre ya muda na tunakwambia umekosea nini na tunakupa muda kurekebisha yale makosa yaliyofanyika,kama unakumbuka zamani Miss Tanzania watu walikua wanapanda na yale mavazi ya ufukweni yakiwa tupu bila kufunga jukwaani lakini taratibu tumewaambia hairuhusiwi kupanda hivyo,kwa sababu ni lazma wakaguliwe wakiwa vile hakuna watazamaji wanaokuwepo kwa muda huo,lakini kabla hatujakufungia tunakupa barua kwamba umekosea A,B,C,D na ufanye marekebisho kwenye hatua hiyo vinginevyo tunakufungia,sasa kama umetuma barua na hakuna kilichorekebishwa pia inakua ni kinyume na utaratibu kwamba tunafika lakini si kila siku sisi huwa tunafika tunawapa wale warembo semina lakini si siku zote wanazokaa kambini sisi tunafika,siwezi kuwa na taarifa bila kuniambia mtu aliekuepo hapo.


No comments:

Post a Comment