STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 6, 2013

Golden Bush Veterani kupeleka maujuzi yao Zenji, kuivaa KMKM J'2

Kikosi cha Golden Bush
TIMU ya Golden Bush Veterans itakuwa na ziara ya siku moja huko Zanzibar kwa mwaliko wa timu ya KMKM Veterans. Tukiwa Zanzibar Golden bush tutacheza mecho moja siku ya jumapili jioni na ndugu zetu wa KMKM katika uwanja wao wa nyumbani. Tukiwa Zanzibar Golden bush tutafikia katika Hotel ya Baraste iliyoko maeneo ya Michenzani karibu kabisa na hotel  iliyokuwa maarufu sana enzi hizo, Bwawani Hotel.

Mipango yote imekamilika na timu yetu iko sawasawa kwa ajili ya mpambano huo ambao utakuwa unafungua ukurasa mpya kabisa wa kutengeneza ushirikiano na ndugu zetu wa Visiwani.

Msafara wa wachezaji wa Golden bush utaanza saa moja kamili asubuhi pale bandarini Dar es salaam huku ukiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi na mambo ya kale bwana Jeremiah Mulungu, Kocha Mkuu Madaraka Selemani “Mzee Wa Kiminyio” Kocha msaidizi bwana Herry Morris, Nahodha wa timu bwana Yahaya Issa na wachezaji wegine wandamizi .

Tukitoka Zanzibar, tutakamilisha taraibu za kuomba  game na timu ya Waheshimiwa Wabunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tuko kwenye hatua za mwisho kabisa za mazungumzo na kocha Mkuu wa timu ya Bunge Mheshimiwa Kassim Majaliwa.

Tunasikitika wapenzi wetu wa Dar es Salaam mtatukosa weekend hii lakini weekend inayofuata tutakuwa jijini kutoa burudani ya soka kwa wapenzi wetu.

Karibuni sana.

No comments:

Post a Comment