STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 6, 2013

Wanamichezo, wasanii wa muziki wamlilia Nelson Mandela


http://umuhanzi.com/IMG/jpg/3_nelson_mandela_boxing_2.jpg
Nelson Mandela enzi za ujana akiwa bondia
WANASOKA na wasanii nyota wa muziki duniani wameonyeshwa kusthushwa na kifo cha Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela aliyefariki usiku wa kuamkia leo kwa kuandika jumbe mbalimbali kuonyesha hisia zao juu ya kifo cha Shujaa huyo wa Afrika.
Nyota kama akina Cristiano Ronaldo, Gerard Pique, Sergio Ramos na wengine wameandika katika akaunti zao za mitandao ya kijamii kuonyesha walivyoguswa na kifo cha Mandele.
Hali hiyo ipo pia kwa wasanii mbalimbali nyota wa muziki duniani kama Rihanna, Akon, Ludacriss, P Diddy na wengine nao walitumia jumbe zao za rambirambi kuhusiana na kifo cha Mzee Mandela aliyekuwa akitibiwa homa ya mapafu nyumbani kwake baada ya kulazwa hospitalini kwa miezi mitatu.
Ebu soma baadhi ya jumbe za wasanii hao kupitia akaunti zao za Tweet uone namna gani Mzee Mandela alivyokuwa maarufu siyo kwenye siasa tu, bali hata kwa watu wa kada nyingine ikikumbukwa kuwa enzi zake aliwahi kuwa mahiri katika mchezo wa ngumi.













 












No comments:

Post a Comment