STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 10, 2013

Ribery, Messi, Ronaldo uso kwa uso 3 Bora ya Ballon d'Or

Ribery anayejaribu bahati yake mwaka huu

'Mfalme' anayeshikilia tuzo hiyo mara nne

Ronaldo akiwa na tuzo ya FIFA ya 2008

Bern, Uswisi
SHIRIKISHO la Soka la Kimataifa (Fifa), limewatangaza rasmi Cristiano Ronaldo, Lionel Messi na Franck Ribery kuwa nyota watatu waliobaki kati ya 10 watakaowania Tuzo ya Mwanasoka Bora wa Mwaka wa Dunia (Ballon d'Or 2013) jana.
Mshambuliaji wa Barcelona na timu ya Taifa ya Argentina, Messi ameibuka kidedea katika tuzo hiyo, ambayo awali ilikuwa ikiitwa Tuzo ya Fifa ya Mwanasoka Bora wa Mwaka wa Dunia, kwa miaka minne mfululizo, wakati mshambuliaji wa Real Madrid, Ronaldo aliitwaa kwa mara ya mwisho katika kura za mwaka 2008.
Licha ya kutotwaa taji lolote kubwa msimu uliopita, Mreno Ronaldo anapewa nafasi kubwa ya kuhitimisha rasmi utawala wa Messi wa kuwa mwanasoka bora wa dunia wakati matokeo yatakapotangazwa Januari 13, mwakani.
Nyota huyo mwenye miaka 28 ameifungia Real Madrid mabao 25 msimu huu na pia alifunga 'hat-trick' ya kusisimua wakati Ureno ikiifunga Sweden katika mechi yao ya mtoano ya kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwakani nchini Brazil.
Messi aliifungia Barcelona mabao 56 msimu uliopita, akiisaidia Barca kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Hispania wakati Ribery akiisaidia Bayern Munich kutwaa taji la Bundesliga (Ligi Kuu ya Ujerumani), Kombe la Ligi na taji la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.
Kocha wa zamani wa Manchester United, Alex Ferguson, Kocha wa Bayern Munich, Jupp Heynkes na Kocha wa Borussia Dortmund, Juergen Klopp wameingia katika nafasi tatu bora 'top 3' ya vinara wanaowania Tuzo ya Kocha Bora wa Mwaka wa Dunia.
Mshambuliaji wa Paris St Germain na timu ya taifa ya Sweden, Zlatan Ibrahimovic alishindwa kuingia katika 'top 3' ya wanaowania Ballon d'Or ingawa anafukuzia tuzo ya Puskas inayotolewa kwa mfungaji wa "bao zuri zaidi la mwaka" kutokana na bao la mbali la 'tik-taka' alilofunga dhidi ya England.
Wote waliongia katika fainali ya kuwania tuzo mbalimbali walithibitishwa baada ya kura kupigwa na manahodha na makocha wa timu za taifa kutoka nchi zote wanachama wa Fifa na wawakilishi wa vyombo vya habari wanaoteuliwa pia na Fifa na jarida la soka la Ufaransa.

No comments:

Post a Comment