STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 10, 2013

Timu zipi kutinga 16 Bora Ligi ya Mabingwa Ulaya?

Juve inayohitaji ushindi ili kutinga 16 Bora
MECHI za hatua ya mwisho za makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya zinatarajiwa kuanza kuchezwa leo na kumalizika kesho ili kujua timu za mwisho za kuingia hatua ya 16 Bora ya ligi hiyo maarufu duniani.
Mpaka sasa ni timu nane tu kati ya 16 zilizojihakikishia hatua hiyo ya mtoano kuwania Robo Fainali, huku nane nyingine zikitarajiwa kujulikana leo na kesho baada ya mechi zao za kufungia makundi yao.
Mabingwa watetezi, Bayern Munich, Chelsea, Manchester City, Manchester United, Real Madrid, Paris St-Germain, Barcelona, na Atletico Madrid.zenyewe tayari zimeshatangulia mapema katika hatua hiyo, huku
Arsenal ikiwa inaonekana kutinga japo bado inatishwa na wapinzani wake, Napoli anaocheza nao na Borussia Dotmund zenye pointi 9, tatu pungu na ilizonazo wao wenyewe 12.
Vigogo vinavyohitajika kutoka jasho ili kutinga hatua hiyo ya mtoano ni pamoja na Juventus na AC Milan, japo zinaonekana zina nafasi kubwa ya kufuzu hatua hiyo inayofuata.


Robin van Persie anatarajia kucheza mechi hii wakati United watakapominyana na Shakhtar Donetsk

RATIBA ILIVYO
LEO Jumanne Des 10, 2013
Manchester United FC v FC Shakhtar Donetsk
Real Sociedad de Fútbol v Bayer 04 Leverkusen
Galatasaray v A.Ş. Juventus
FC København v Real Madrid CF
SL Benfica v Paris Saint-Germain
Olympiacos v FC RSC Anderlecht
FC Bayern München v Manchester City FC

Viktoria Plzeň v PFC CSKA Moskva

KESHO Jumatano Des 11, 2013
FC Schalke 04 v FC Basel 1893
Chelsea FC v FC Steaua Bucureşti
Olympique de Marseille v Borussia Dortmund
Napoli v Arsenal FC
FK Austria Wien v Football Club Zenit
Club Atlético de Madrid v FC Porto
AC Milan v AFC Ajax
FC Barcelona v Celtic Fc

No comments:

Post a Comment