STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 23, 2014

Hivi ndivyo roho za madenti watano zilivyopotea Mtwara

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mtwara, Zelothe Stephen, akiwa ndandi ya  wodi namba moja katika Hospitali ya mkoa ya Ligula, alipokwenda kuwaona majeruhi wa ajali  ya  wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mustafa Sabodo, iliyotokea jana katika barabara ya Mtwara Lindi wakati wanafunzi wa shule hiyo wakikimbia mchakamchaka asubuhi. Kushoto Kaimu Katibu tawala wa Mkoa Smythies Pangisa. Katika ajali hiyo iliyohusisha gari ndogo aina ya Mercedes Benz lenye namba za usajili T174 AEB imesababisha vifo vya wanafunzi wanne na wengine 47 kujeruhiwa
 Mmoja wa majeruhi akipelekwa wodini baada ya kupokewa katika hospitali hiyo
 Kamanda wa Polisi, Zelothe Steven akizungumzia ajali hiyo
Kamanda Zelote akikagua gari lililohusika katika ajali hiyo 
 
Wanafunzi wanne wa Shule ya Sekondari ya Mustapha Sabodo iliyoko katika kijiji cha Msijute Halmashauri ya Mtwara Vijijini, mkoani Mtwara wamekufa papo hapo baada ya kugongwa na gari wakati wakikimbia mchakamchaka jana alfajiri.

Wanafunzi hao walikufa baada ya kugongwa na gari aina ya Mercedes-benz namba T174 AED jirani na eneo la shule.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Zelothe Stephen, alisema jana kuwa ajali hiyo ilitokea alfajiri saa 11:40 katika maeneo ya shule hiyo barabara kuu ya Dar es Salaam-Lindi na kwamba gari hilo lililokuwa katika mwendo wa kasi, lilikuwa linaendeshwa na Baraka Mgengwe (50) wakati likitokea Mtwara kwenda Lindi.

Kamanda Stephen hakutoa maelezo zaidi kuhusiana na mazingira ya ajali hiyo, mbali ya kusema kuwa wanafunzi hao walipatwa na mkasa huo wakati wakigeuka kurejea shuleni.
Alisema kuwa wanafunzi 21 walijeruhiwa huku wengine 26 waliopata mshtuko, walitibiwa kisha kuruhusiwa.
 

No comments:

Post a Comment