STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 6, 2014

Liverpool yaduwazwa ugenini, ubingwa kwao ni majaliwa sasa!

Hekaheka uwanjani kati ya Crystal Palace na Liverpool jana
Liverpool wakipongezana baada ya kufunga moja ya mabao yao matatu

Suarez akioyesha makali yake kabla ya kufuga bao la tatu la Liverpool
MBIO za kuelekea kunyakua ubingwa wa Ligi Kuu England baada ya miaka 24 kupita kwa Liverpool imekutana na vikwazo baada ya usiku wa jana kung'ang'aniwa na timu ya Crystal Palace na kutoka sare ya mabao 3-3, huku Suarez akizidi kutikisa nyavu akifikisha bao la 31.
Liverpool waliokuwa ugenini walifanikiwa kuongoza zaidi ya nusu ya mchezo huo wakiwa mbele kwa mabao 3-0, lakini cha ajabu mabao yote yalikuja kurejeshwa na wenyeji na kufanya wagane pointi moja moja, ambazo zinawarejesha Liverpool kileleni lakini wakiweka rehani matumaini yao ya ubingwa msimu huu.
Wageni walianza kuandika bao la kuongoza lililofungwa na Joe Allen katika dakika ya 18 kwa kumalizia kazi nzuri ya nahodha wake, Steven Gerrard na kudumu hadi wakati wa mapumziko.
Dakika nane baada ya kuanza kwa kipindi cha pili Daniel Sturridge aliifungia Liverpool bao la pili kabla ya dakika mbili baadaye Suarez kufunga bao lake la 31 katika msimu huu na kuifanya timu yake iongoze kwa mabao 3-0.
Hata hjivyo wenyeji walicharuka na kurejesha mabao hayo kupitia kwa Delaney aliyefunga dakika ya 79 na Gayle aliyefunga mabao mawili katiika dakika ya 81 na 88 na kuiduwaza Liverpool ambao wamesaliwa na mchezo mmoja,huku wapinzani wao,Manchester City waliowaoindoa kileleni kwa sare hiyo ya jana wamesaliwa na mechi mbili wakiwa na pointi 80.
Ligi hiyo itaendelea tena leo kwa pambano moja kati ya Manchestert United iliyotoka kupokea kipigo cha baoa 1-0 toka kwa Sunderland itakapoumana na Hull City.

No comments:

Post a Comment