STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 6, 2014

Network Love ya Ruvu Stars videoni

Kiongozi wa Ruvu Stars, Khamis Amigolas
BENDI ya muziki wa dansi ya Ruvu Stars keshokutwa inatarajia kuanza kurekodi video za nyimbo zao tatu ambazo zinaendelea kutamba kwenye vituo mbalimbali vya redio nchini.
Akizungumza na MICHARAZO mmoja wa viongozi wa bendi hiyo ya maafande wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Rogart Hegga 'Katapila' alisema kuwa video hiyo itahusisha nyimbo zao za 'Network Love', 'Spirit' na 'Jua Kali' ambazo ndizo zilizolitambulisha kundi hilo kwa mashabiki wa muziki baada ya kusukwa upya likiwahusisha wanamuziki mahiri nchini.
Baadhi ya wanamuziki walionyakuliwa na kundi hilo ili kulisuka upya ni pamoja na Hegga, Khamis Kayumbu 'Amigolas', Khadija Mnoga 'Kimobitel', Jojo Jumanne, Victor Nkambi na rapa Msafiri Diouf.
Hegga alisema kazi hiyo ya kurekodi video hizo itaanza wiki hii na zoezi hilo litakapomalizika wataingia studio kumalizia nyimbo zao tatu za mwisho za kukamilisha albamu yao ya kwanza waliyopanga kuizindua baadaye mwaka huu.
"Tumesitisha zoezi la kumalizia nyimbo zetu tatu za kuhitimisha albamu ili kurekodi video za nyimbo za awali na kazi hiyo itafanywa katikati ya wiki chini ya kampuni moja ya jijini Dar es Salaam," alisema Hegga.
Alisema nyimbo za mwisho walizokuwa wameanza kurekodi ni 'Kioo' utunzi wake kiongozi mkuu wa bendi hiyo, Khamis Amigolas, 'Chewa Original' wa Seleman Muhumba na 'Facebook' wa Mkuu wa Jukwaa, Victor Nkambi ambaye pia ni 'mpapasa' kinanda mahiri nchini.

No comments:

Post a Comment