STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 6, 2014

Matumla, Miyeyusho kuyeyushana Jumamosi PTA

Miyeyusho na Matumla wakiwa katika pozi. Wawili haowatapigana siku ya Jumamosi pale PTA
MABONDIA Francis Miyeyusho 'Chichi Mawe' na mtoto wa bingwa wa zamani wa dunia, Rashid Matumla, Mohammed Matumla 'Snake Boy Jr' watapanda ulingoni siku ya Jumamosi kuchapana katika pambano lisilo la ubingwa.
Aidha, mabondia hao wanatarajiwa kupima uzito na afya zao siku ya Ijumaa kwenye ukumbi wa Mango Garden, Kinondoni kabla ya kuvaana siku inayofuata kwenye ukumbi wa PTA, jijini Dar es Salaam.
Mabondia hao awali walipangwa kupigana Aprili 26, lakini likasogezwa mbele ili kupisha pigano la Miyeyusho dhidi ya Mthailand Sukkasem Kietyngyuth ambaye alimchapa Miyeyusho kwa TKO ya raundi ya kwanza.
Akizungumza na MICHARAZO, Rais wa TPBO-Limited inayosimamia pambano hilo, Yasin 'Ustaadh' Abdallah alisema pambano hilo lipo kama lilivyopangwa siku ya Mei 10.
Ustaadh alisema mabondia wote wapo kambini kujiandaa kwa ajili ya pambano hilo la kukata mzizi wa fitina baina yao baada ya kuwapo kwa tambo za muda mrefu. Miyeyusho amejichimbia mjini Bagamoyo na mpinzani wake yuko jijini Dar.
Rais huyo wa TPBO-Limited alisema maandalizi ya pambano hilo lililoandaliwa na promota Ally Mwazoa na litakalokuwa na michezo kadhaa ya utangulizi, yanaendelea vizuri.
Ustaadh alisema mapambano ya utangulizi siku hiyo yatakuwa kama ifuatavyo; Simon Zablon dhidi ya Keis Amary (kg 60), Mane Patrick dhidi ya  Sadiq Abdul (kg 50), Kassim Gamboo dhidi ya Kassim Rajab (Kg55), Azizi Abdallah atapigana na Ide Mnali (kg 60) na mkongwe Rashid Ally dhidi ya Suma Ninja (kg 60).

No comments:

Post a Comment