STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 13, 2014

Balotelli kutua Arsenal kwa msaada wa Puma

KAMPUNI ya usambazaji wa vifaa vya michezo, Puma itaisaida Arsenal kufanikisha mpango wa kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Italia, Mario Balotelli kutoka AC Milan.

Mpachika mabao huyo anadhaminiwa na Puma, ambao pia mapema Januari walitangaza kuidhamini Arsenal.

Mustakabali wa Balotelli ndani ya Milan uko shakani baada ya Rais Silvio Berlusconi kusema bado hajaamua lolote kuhusu mchezaji huyo na mchambuzi wa Sky Sport nchini Italia, Mario Giunta akaandika: "Arsenal inamtaka sana Balotelli na Arsene Wenger atafanya kitu chochote kumhamishia London. 
Kutua kwa mshambuiliaji kwa Wapiga Mitutu hao wa Londo kutakuwa msaada mkubwa katika safu ya ushambiuliaji inayomtegemea Oliver Giroud.

No comments:

Post a Comment