STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 13, 2014

Neymar aiongoza vyema Brazil, yaitungua Croatia 3-1

20140613-010343-3823241.jpg












WENYEJI wa michuano ya Fainali za Kombe la Dunia, Brazili imeanza vyema fainali hizo kwa kuicharaza Croati kwa mabao 3-1, huku nyota wa timu hiyo na blabu ya Barcelona, Neymer akifunga mabao mawili moja likiwa la penati iliyolalamikiwa na wageni.
Goli jingine la Brazili lilifungwa na Oscar dakika za lala salama, baada ya awali kutanguliwa na bao la kujifunga la Marcelo dakika ya 11 ya mcvhezo huo ulioptanguliwa na sherehe za ufungizi zilizofana.
Ushindi huio umeiweka Brazil katika nafasi nzuri ya kuwatuliza mashabiki wao ambao wamekuwa hawana amani na timu yao na hasa kutawaliwa na vurugu za watu wanaopinga michuano hiyo kufanyika nchini kwao kwa madai ni gharaa kubwa ambazo fedha zilizotumika kuandaa zingewasaidia katika huduma za kimaendeleo.
Michuano hiyo itaendelea tena leo saa 1 usiku kwa saa za Afrika Mashariki kati ya Mexico dhidi ya wawakilishi wa Afrika Cameroon kabla ya timu za Uholanzi kuvaana na mabingwa watetezi Hispania baadaye.

No comments:

Post a Comment