STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 12, 2014

Rais TAFF amwagiwa sifa kwa kujitolea


RAIS wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) Simon Mwakifamba amemwagiwa sifa kwa kuwa mwepesi wa kujitolea kuwasaidia wasanii wenye matatizo, huku wasanii wengine wakiombwa kuiga mfano wake bila kujali uwezo wa mtu wa kifedha.
Pongezi hizo zimetolewa kwenye msiba wa Mzee Small kutokana na namna Rais huyo wa TAFF alivyokuwa akihaha kuweka mambo sawa huku wasanii wa Bongo Movie wakiwa hawapo kwenye eneo hilo mpaka walipokuja baadaye majira ya mchana.
"Kwa kweli Rais wa TAFF, ni mtu wa watu anajitolea na amekuwa mwepesi kila wasanii wanapopatwa na shida ni mfano wa kuigwa na kufahamu wajibu wake kama kiongozi, wasanii wote wangekuwa hivi mambo yangekuwa mazuri sana," alisema mmoja wa wasanii wakiongwe aliyeomba kuhifadhiwa jina lake aliyekuwa msibani hapo mapema.
Mdau mwingine wa sanaa, alisema tofauti na wasanii wa Bongo Movie ambao huchagua aina ya misiba au wasanii wa kuwasaidia hali ni tofauti kwa uongozi wa TAFF na hasa Rais wake na baadhi ya waigizaji
wakongwe wakitajwa kwa majina, Dk Cheni, Chiki Mchoma, Monalisa na mama yake.

No comments:

Post a Comment