STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 12, 2014

Baby Madaha ala 'shavu' Kenya

NYOTA wa filamu na muziki wa Tanzania anayefanya kazi zake nchini Kenya, Baby Madaha amelamba 'shavu' nono kupitia kampuni ya simu ya Safaricom.
Akizungumza na MICHARAZO toka nchini humo, Baby Madaha aliyeachia wimbo mpya uitwao 'Nawaponda' alisema karibu mwezi mmoja sasa anafanya 'tour' chini ya Safaricom, jambo alilofichua limempa ulaji mkubwa na kujitambulisha zaidi nchini humo.
"Nipo kwenye 'tour' ya Safaricom, ambapo napiga shoo sambamba na kuitangaza kampuni kwa kweli nashukuru sana kufanya kazi chini ya Candy n Candy', " alisema Baby.
Msanii huyo hata hivyo hakuweka bayana mkataba alioingia na kampuni hiyo maarufu ya simu za mkononi nchini humo, ila alidai ni mnono na kwamba umemfanya kujivunia kuwa msanii anayefanya kazi nchini Kenya.

No comments:

Post a Comment