STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 11, 2014

Msiba mwingine soka la Bongo, beki wa zamani atunaye

Na Salum Vuai, ZANZIBAR
WAKATI Nahodha wa zamani wa KMKM, Ali Issa Simai 'Kapteni' aliyefariki juzi na kuzikwa jana visiwani Zanzibar, jahazi la michezo limeendelea kupata majonzi mengine kufuatia kifo cha nyota wa zamani wa Pilsner, Abdallah Sumbwa.
Sumbwa alikumbwa na mauti hayo mchana wa jana kutokana na tatizo la Saratani ya Tumbo na anatarajiwa kuagwa leo kabla ya kusafrishwa kwenda kuzikwa kwao Kilosa, Morogoro.
Kwa mujibu wa taarifa ambazo MICHARAZO imezipata usiku wa jana zilisema kuwa mchezaji huyo alikuwa amelazwa hospitali ya Ocean Road na kukumbwa na mauti saa 8 mchana.
Msiba wa mchezaji huyo upo nyumbani kwake Buguruni na inaelezwa atasafirishwa leo kwenda kuzikwa kijijini wao mijini Kilosa, Morogoro.
Msiba huo umekuja wakati visiwani Zanzibar jana ulishuhudia ukimzika Kapteni aliyeugua ghafla,
Marehemu, alikutwa na mauti nyumbani kwake Fuoni baada ya kurudi kutoka katika shughuli zake za kawaida nyakati za Magharibi na alizikwa jana. Chukwani.
Jeneza lililobeba mwili wa marehemu Ali Issa Simai (katika picha ndogo) likipelekwa mazikoni leo

Mmoja wa wanasoka waliocheza pamoja naye Abdalla Maulid, amenukuliwa na Bin Zubeiry kuwa, marehemu alikuwemo kwenye kikosi cha washika magendo hao kilichoshiriki michuano ya klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati mwaka 1974 yaliyofanyika mjini Dar es Salaam, yakiwa katika mwaka wake wa kwanza.

Maulid alifahamisha kuwa, mwaka 1975, kepteni huyo aliitwa katika timu ya taifa ya Zanzibar iliyoshiriki mashindano ya Chalenji kwa vijana, yaliyofanyika uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam, na ubingwa kuchukuliwa na Kenya.

Aidha mwaka huo wa 1975, marehemu aliyesifika kwa umahiri wake wa kumiliki mpira na mbinu za kufumania nyavu, aliteuliwa katika timu kubwa ya taifa iliyokuwa chini ya kocha Muingereza George Dunga.

Pamoja na kuibeba vyema klabu yake katika ligi kuu ya muungano kuanzia mwaka 1976 na kufanikiwa kutwaa ubingwa mwaka 1984, marehemu Ali Issa pia aliisaidia Navy (sasa KMKM) kucheza klabu bingwa Afrika mwaka 1978, ambapo walifika hatua ya nne bora.

Nahodha huyo alidumu na KMKM hadi mwaka 1990 alipoamua kutundika madaluga, na kuendelea kuchezea timu ya maveterani, Wazee Sports.

Mazishi ya marehemu huyo aliyeacha watoto kumi, yalihudhuriwa na mamia ya wananchi na wanamichezo mbalimbali, ambapo mwili wake ulisaliwa katika msikiti uliopo karibu na uwanja wa Amani, na baadae kupelekwa malazoni Chukwani. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu pahala pema Peponi. Amin.

No comments:

Post a Comment