STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 11, 2014

Ureno yainyuka Ireland, Ronaldo akirejea dimbani

URENO jana iliendelea kudhihirisha dhamira yao ya kufanya kweli kwenye Kombe la Dunia baada ya kuikanyaga timu ya Jamhuri ya Ireland kwa mabao 5-1 katika mechi ya mwisho ya kujiandaa na michuanio hiyo ya Brazil inayoanza kesho.
Ureno waliopangwa kundi G na timu za Ujerumani watakaoanza nao vita Juni 16, Ghana na Marekani huo ni ushindi wake wa pili mfululizo bnaada ya wiki iliyopita kuinyoa Mexico bao 1-0 katike mechi kama hiyo ya maandalizi.
Katika mchezo huo wa jana nyota wa timu hiyo na klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo alicheza kwa dakika 65 na kudhihirishia mashabiki wa Ureno kuwa yupo fiti tayari kulipaisha taifa hilo.
Ureno ilianza kuhesabu bao la kwanza dakika ya pili ya mchezo huo kupitia Hugo Almeida kwa pasi ya Silvestre Varela kabla ya Keogh kujifunga dakika ya 20 na kuipa Ureno uongozi wa 2-0 na kwenye dakika ya 37 Hugo Almeida alirejea tena nyavuni , mabao yaliyodumu hadi wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili kilianza kwa wenyeji kujipatia bao lao pekee la kufutia machozi dakika ya 52 kupitia McClean kabla ya Vieirinha kufunga bao la nne dakika ya 77 kwa pande la Nani ambaye pia alimtengenezea mpira Fabio Coentrao kufunga bao la tano kuhitimisha ushindi huo mnono kabla ya kuwakabili Ujerumani wiki ijayo kwenye Fainali za Kombe la Dunia.

No comments:

Post a Comment