STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 11, 2014

Wambura arejeshwa uchaguzi wa Simba?!

Michael Wambura
HATMA ya Michael Wambura kurudishwa au kutoswa kwenye kugombea urais Simba inatarajiwa kufahamika leo wakati Kamati ya Rufaa ya TFF itakapotoa taarifa yake kwa wanahabari.
Hata hivyo habari za chini ya kapeti zinadai kuwa Wambura amepeta baada ya maamuzi ya rufaa yake kuamuliwa kwa kura.
Wambura alikata rufaa kupinga kuenguliwa kwenye kinyang'anyiro hicho kitakachofanyika Juni 29 na kwamba Kamati ya rufaa ya TFF, kupitia mwenyekiti wake, Julius Lugaziya imemrudisha, ila tarifa rasmi zitatolewa leo saa 5 asubuhi.
Kama tetesi hizo zitakuwa sahihi basi ni kwamba  Wambura atapambana na Avens Aveva kwenye kinyang’anyiro cha kuwania urais wa klabu maarufu ya Simba.
Awali, Wambura aling’olewa kuwania urais baada ya kubainika uanachama wake una walakini.
Kamati ya uchaguzi ya Simba chini ya mwanasheria maarufu, Dokta Damas Daniel Ndumbaro ilibaini kuwa uanachama wake una walakini na mkutano mkuu wa Simba pekee ndiyo wenye uwezo wa kurekebisha jambo hilo.

No comments:

Post a Comment