STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 11, 2014

Shilole: Tuombe na kufunga sana hali tete

NYOTA wa muziki na filamu nchini, Zuwena Mohammed 'Shilole' amewataka wasanii wenzake na Watanzania kwa ujumla kufunga na kuomba Mungu ili awanusuru na majanga ambayo yamekuwa yakiongezeka kila uchao kiasi cha kuwapa hofu ya maisha.
Aidha ameendelea kuomboleza vifo vya wasanii na wadau wa filamu vilivyotokea akisisitiza kuwa hiyo ni kazi ya Mungu na asisakwe mchawi kwani ni sawa na kukufuru.
Akizungumza na MICHARAZO alisema kwa hali ya mambo yanayozidi kuwaandama wasanii na taifa kwa ujumla ni muda mwafaka kwa kila mtu kwa imani yake kufunga na kumuomba Mungu afanye wepesi katika mitihani anayowapa.
Shilole anayetamba na wimbo wa 'Chuna Buzi' alisema kumekuwa na matukio ya kuhuzunisha na kuogopesha kama ya watu kuchinjana, watoto kufanyiwa vitendo vya ukatili mbali na vifo vya kushtukiza vya wasanii na wanamichezo, kitu alichosema ni vyema kila mtu kwa imani yake kufunga na kuomba Mungu awanusuru.
Kauli ya Shilole imekuja siku chache baada ya vifo mfululizo vya wasanii na wanamichezo ambavyo vimewafanya wadau wake wasipumue.
Kwa wiki mbili vimeshuhudiwa vifo vya watu saba, akiwamo Amina Ngaluma, Adam Kuambiana, Rachel Haule, George Tyson, Gebo Peter, Mzee Small na Kanali Ally Mwanakatwe waliofariki mwishoni mwa wiki.

No comments:

Post a Comment