STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, September 9, 2014

Diamond, Yami Alade kuangusha ya pamoja Coke Studio Africa

STAA wa Mdogomdogo na My Number One, Diamond Platnumz amerejea tena kwenye msimu wa pili wa kipindi cha Coke Studio Africa na awamu hii atatangeneza 'pea' na mkali wa Johnny, Yemi Alade kutoka nchini Nigeria.
Kwa mujibu wa taarifa za kwenye mtandao, Diamond ni msanii wa nne mwaka huu kutoka Tanzania aliyeshiriki kwenye kipindi hicho kinachorekodiwa jijini Nairobi, Kenya.
Wengine waliowahi kushiriki ni pamoja na Vanessa Mdee aliyerekodi na Burna Boy wa Nigeria, Joh Makini aliyerekodi na Chidinma wa Nigeria na Shaa aliyerekodi na Jacky Chandiru wa Uganda.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Yemi aliyekuja nchini hivi karibuni aliweka picha yake akiwa na Diamond katika na kudokeza anavyojisikia furaha kufanya kazi na mshindi huyo wa tuzo saba kwa mpigo wa Kili Music Awards-2014.
#wonderment! With the infamous ubertalented six-abbs superstar Diamond….@diamondplatnumz
#iAmHumbled #thankYouCokeStudio, ForThe Opportunity God bless AFrica.. #cokeastudioafrica
@cokestudioafrica @dresomes Nosa @chocolatecity
Diamond has been singing your song all morning@audumaikori.
Naye Diamond katika picha akiwa na mrembo huyo
ameandika:
Na dem ake Johny @yemialade , ushaelewa nini kinaendelea si eti????….. (jus me and Johny’s
Girlfriend…You allready know what it is ryt???… Cc@yemialade

No comments:

Post a Comment