STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, September 9, 2014

Hispania yaifumua Macedonia 5-1 bila Diego Costa, David Silva nouma

Silva na Paco Alcacer wakipongezana baada ya kinda hilo (9) kufunga bao
Breaking away: Cesc Fabregas escapes a challenge from Macedonian midfielder Stefan Spirovski as Spain exerted their authority in the midfield areas
Utanivunja nyonga bure! Mtaalam Cesc Fabregas akimpeleka mtu chini
MABINGWA watetezi wa Kombe la Mataifa ya Ulaya, Hispania ikiwa bila mshambuliaji wao nyota Diego Costa anayesumbuliwa na majeraha ya nyama za Paja, usiku wa kuamkia leo ilitoa onyo kwa wapinzani wake baada ya kuifumua Macedonia kwa mabao 5-1 katika mechi za kuwania fainali hizo za Uero 2016.
Mchezaji aliyechukua nafasi ya Costa, Paco Alcacer , 21 aliitenda haki kwa kuifungia Hispania bao la pili katika dakika ya 17 akimalizia krosi pasi safi ya Cesc Fabregas.
Bao la kwanza la wababe hao wa zamani wa Dunia, lilitumbukizwa wavuni na Sergio Ramos  kwa panalti dakika ya 16 baada ya David Silva kuangushwa kwenye eneo la hatari.
Macedonia walijipatuia bao lao la kufutia machozi katika dakika ya 28 baada ya Juanfran kufanya madhambi na Agim Ibraimi akafunga kwa kumtungua Iker Casillas.
Sergio Busquets aliiandikia Hispania bao la tatu sekunde chache kabla ya kwenda mapumziko, huku mabao mengine ya ushindi huo mnono kwa Hispania yakiwekwa kimiani na David Silva katika dakika ya 50 na Pedro aliyepigilia msumari dakika za lala salama.

No comments:

Post a Comment