STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 5, 2014

Kivumbi Afrika, mbio za kuwania tiketi ya Morocco zaanza rasmi

https://media.premiumtimesng.com/wp-content/files/2014/06/Eagles-Getty-images.jpg
Mabingwa Watetezi, Nigeria
http://level3.soccerladuma.net/cms2/image_manager/uploads/News/160996/7/default.jpgMBIO za kuwania kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2015 hatua ya makundi zinatarajiwa kuanza kutimua vumbi leo ambapo nchi 28 zitakuwa zikitafuta nafasi 15 kwa ajili ya kujiunga na mwenyeji Morocco katika michuano hiyo Januari mwakani. 
Kuelekea katika michuano hiyo suala kubwa lililokuwa limetawala ni juu ya viwanja vitakavyotumika kwa baadhi ya mechi kutoka na wasiwasi wa ugonjwa hatari wa Ebola. 
Shirikisho la Soka barani Afrika-CAF limeziamuru nchi za Guinea na Sierra Leone kuhamisha mechi zao za nyumbani katika viwanja huru kwasababu ya mlipuko wa ugonjwa huo kwenye nchi hizo. 
Guinea wao wamehamishia mechi yao ya kundi E dhidi ya Togo huko Casablanca nchini Morocco huku wakikabiliwa na majeruhi kadhaa katika kikosi chao akiwemo Florentin Pogba ambaye ni kaka mkubwa wa nyota wa kimataifa wa Ufaransa Paul Pogba. 
Pogba alipata majeruhi wakati klabu ya ya Saint Etienne ilipochabangwa kwa mabao 5-0 na mabingwa wa Ufaransa Paris Saint Germain Jumapili iliyopita. 
Guinea pia itawakosa kiungo wa Lorient Abdoulaye Sadio Diallo na mshambuliaji wa Lyon Mohamed Lamine Yattara wakati wapinzani wao Togo wao watakuwa na ahueni baada ya mshambuliaji Emmanuel Adebayor kurejea katika majukumu ya kimataifa baada ya kukosekana kwa miezi 18. 
Mechi nyingine itakayochezwa baadae leo utakuwa mchezo wa kundi E utakaozikutanisha Senegal na Misri jijini Dakar. 
Washindi wawili kutoka katika kila kundi watafuzu na kuungana na Morocco katika fainali za Afcon Januari mwakani.
RATIBA YA LEO
Sudan    vs   South Africa 
Guinea   vs   Togo
Senegal  vs   Egypt 

KESHO:
DR Congo vs  Cameroon 
Ethiopia  vs   Algeria
Zambia    vs  Mozambique 
Niger    vs  Cape Verde
Nigeria vs  Congo
Burkina Faso  vs  Lesotho
Gabon  vs   Angola   
Ghana   vs  Uganda 
Côte d'Ivoire vs Sierra Leone
Mali vs Malawi 
Tunisia vs  Botswana

No comments:

Post a Comment