STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 5, 2014

Rasmi! Marcos Rojo sasa ruksa kukipiga Manchester United

http://www.laacib.net/wp-content/uploads/2014/08/Rojo21.jpg 
WANACHEKAAA! Ndivyo unavyoweza kusema kwa mashabiki wa Manchester United, baada ya beki wao mpya Marcos Rojo kupata kibali cha kuanza kuitumikia timu hiyo.
Beki huyo  anaweza kuichezea kwa mara ya kwanza klabu yake hiyo katika mchezo wa Ligi Kuu ya England dhidi ya Queens Park Rangers Uwanja wa Old Trafford Septemba 14 baada ya kupatiwa hati ya kufanya kazi.
Rojo alisafiri hadi Lisbon Alhamisi ili kukamilisha taratibu za kupata hati hiyo ya kufanyia kazi England.
Kufanikiwa kwa mchezaji huyo kupata hati hiyo ya kufanyia kazi ni faraja kwa kocha Louis van Gaal, ambaye kikosi chake mina tatizo la safu ya ulinzi.

No comments:

Post a Comment