STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 5, 2014

RONALDO AFUNGUKA, ADAI ATAREJEA TENA OLD TRAFFORD

http://media1.santabanta.com/full1/Football/Cristiano%20Ronaldo/cristiano-ronaldo-16h.jpgMSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo amesisitiza shauku yake ya kurejea katika klabu ya Manchester United katika siku zijazo. 
Nyota huyo wa kimataifa wa Ureno alifurahia kipindi cha mafanikio wakati akiwa Old Trafford kati ya mwaka 2003 na 2009 kabla ya kuondoka United na kwenda Madrid kwa kitita kilichovunja rekodi cha paundi milioni 94. 
Hata hivyo, Ronaldo, 29 bado amekuwa na kumbukumbu nzuri kwa klabu yake hiyo ya zamani na anatamani siku moja kurudi huko alipojitengenezea jina lake. 
Akihojiwa Ronaldo amesema anaipenda United na kila mtu anajua hilo amelisema mara nyingi sababu kubwa inayomfanya asiisahau klabu ni marafiki aliowaacha na mashabiki ambao walikuwa wakimpa ushirikiano wa kipekee. 
Nyota huyo aliendelea kudai kuwa kwasasa ana furahia kuwepo Madrid na bado ana mkataba wa miaka minne lakini amedai kuwa hawezi kujua kinachoweza kutokea huko mbele.
Mkali huyo anaamini kuna siku atarejea tena kukipiga Old Trafford kulikomwezesha kuitendea haki namba 7 ambayo hivi karibu imepewa Muargentina, Angel di Maria aliyekuwa akicheza nae Santiago Bernabeu.

No comments:

Post a Comment