STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, October 13, 2014

ARSENAL MAJANGA, MAJERUHI WAZIDI KUONGEZEKA

http://img.bleacherreport.net/img/images/photos/003/042/640/hi-res-a01b8eaefd6aaec9613b24d358507950_crop_north.jpg?w=630&h=420&q=75KLABU ya Arsenal imezidi kupata pigo baada ya nyota wake kadhaa kupata majeraha, kufuatia kuumia kwa beki Laurent Koscielny aliyelazimika kujiondoa kwenye mazoezi ya timu yake ya kitaifa ya Ufaransa.
Beki huyo wa kati amejitoa Les Blues kutokana na maumivu ya ukano wa kisigino.

Meneja Arsene Wenger amepigwa na pigo moja baada ya lingine ikiwa ni mechi saba tu ndani ya msimu mpya huku ambapo sasa Koscielny anajiunga na nyota wenzake Danny Welbeck, Mathieu Debuchy, Mikel Arteta, Olivier Giroud, David Ospina, Aaron Ramsey na Yaya Sanogo kwenye zahanati.

Siku mbili baada ya Ujerumani kutangaza kiungo nyota Mesut Ozil atalazimika kutocheza kati ya wiki 10 na 12, Wenger ameongezewa tumbo joto na habari kuwa beki Koscielny amejiondoa kutoka mechi za Ufaransa dhidi ya Ureno na Armenia kwenye msururu wa kufuzu Kombe la Euro la 2016, huku Danny Welbeck naye akiiumia wakati England ikishinda 1-0.
Shirikisho la Ufaransa limeandika kwenye anwani yao ya mtandao wa kijamii wa Twitter kuwa Koscielny anauguza uvimbe wa ukano wake wa kisigino.

No comments:

Post a Comment