STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 28, 2014

Tanzia! Muimbaji Issa Nundu afariki, kuzikwa leo Moshi

Issa Nundu wa tatu toka kulia akiwa na wanamuziki wenzake wa Marquiz
MUIMBAJI nyota wa zamani aliyewahi kuzifanyia kazi bendi kadhaa zikiwamo Orchestra Marquis, MK Group, Makassy, Le Capital Wazee Sugu amefariki katika hospitali ya KCMC Moshi.
Issa ambaye alianza kuugua muda mrefu na kukutwa na tatizo la kusinyaa ubongo, aliamua kurudi kwao Kongo, lakini alipofika Kigoma alizidiwa na kulazwa huko ambako alihamishiwa KCMC Moshi kwa matibabu zaidi. 
Issa ambaye jina lake halisi ni Jackson Issa Nundu atazikwa Moshi leo Jumanne ikiwa taratibu zote zitakamilika. 
Marehemu ameacha mke na watoto kadhaa,
Mungu Aiweke Roho ya Marehemu Issa Nundu Mahali Pema. Ameen

No comments:

Post a Comment