STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 26, 2015

Arsenal 'Majanga' yafa nyumbani 3-1 kwa Monaco

Monaco are jubilant after Kondogbia fired the Ligue 1 outfit into a lead which they never looked like relinquishing
Monaco wakishangilia moja ya mabao yao waliyoitungua Arsenal
Dimitar Berbatov rolled back the years with a glorious finish after Anthony Martial hit Arsenal on the break with a classic counter-attack
Berbatov akiitungua Arsenal
Mtokea benchi Chamberlain akiifungia Arsenal bao la kufutia machozi
Olivier Giroud akikosa bao la wazi kwa kupaisha mpira wa kichwa
Mwenye bahati ya kuwaua Arsenal, Dimitar Berbatov akishangilia bao lake
KLABU ya Arsenal ya Uingereza imejiweka katika nafasi finyu ya kufuzu Robo Fainali baada ya kupokea kipigo cha mabao 3-1 ikiwa nyumbani toka kwa Monaco ya Ufaransa.
Arsenal wakiwa uwanja wa Emirates mjini London, walitawala pambano hilo, lakini Wafaransa waliwapeleka puta na kuandika mabao hayo yaliyowapa nafasi kubwa ya kusonga mbele katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Geoffrey Kondogbia aliifungia Monaco bao la kuongoza katika dakika ya 38′, goli lililodumu hadi wakati wa mapumziko kabla ya Dimitar Berbatov kukwamisha bao la pili kimiani katika dakika ya 53.
Wenyeji walijitutumua na kufunga bao la kufutia machozi dakika ya 90 kupitia kwa Alex Oxlade Chamberlain kabla ya Yannick Ferreira-Carrasco kumkatisha tamaa Arsene Wenger kwa bao la dakika za lala salama.
Kwa matokeo hayo, Arsenal wanahitaji ushindi wa mabao 3-0 ugenini ili kuweza kuitoa Monaco.

No comments:

Post a Comment