STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 26, 2015

Madonna akipiga mwereka jukwaani akitumbuiza London

madonna
Muunganiko wa picha zilizochapishwa katika Daily Mail zikimuonyesha Madonna akiwa chini baada ya kuanguka wakati wa kutumbuiza
She fell over: Madonna still had a look of composure when she knew she was heading for the bottom of the stepsLONDON, England
NYOTA wa muziki wa Pop duniani, Madonna amejikuta akipiga mwereka akiwa jukwaani wakati wa kutumbuiza katika hafla za utoaji wa tuzo za muziki za BRIT 2015.
Muimbaji huyo alipiga mweleka kutoka jukwaa na kuangukia mgongo baada ya mcheza shoo wake mmoja kuvuta `shela’ (mfano wa kofia ndefu aliyoivaa kutoka kichwani) mwanzoni mwa onesho hilo.
Hata hivyo, mwanamuziki huyo mkongwe alikuwa fiti na alirejea tena stejini na kumalizia kibao chake, `Living For Love’.
Baadae mwanamuziki huyo alitoa taarifa rasmi na kusema kuwa "yuko fiti" na `shela’ lake hilo lilikuwa limebana sana.
Tukio hilo la kusikitisha lilitokea mwishoni mwa hafla hiyo ambayo Ed Sheeran na Sam Smith wote walishinda tuzo.

No comments:

Post a Comment