STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 26, 2015

Atletico Madrid na Torres wao wafa Ujerumani

The Spanish striker continues his protests as he asks the official behind the line why his goal was ruled out
MABINGWA wa Hispania, Atletico Madrid wakiwa uwanja wa ugenini walikumbana na kipigo cha bao 1-0 toka kwa wenyeji wao Bayer Leverkusen katika mechi ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Bao pekee la washindi liliwekwa kimiani na Hakan Calhanoglu dakika ya 57.
Dakika ya 75 Fernando Torres 'El Nino' aliipatia Atletico bao la kichwa lakini lilikataliwa na mwamuzi Pavel Kralovec kutoka Jamhuri ya Czech na kumzonga.
Katika pambano hilo wenyeji walionyesha kiwango cha hali ya juu cha soka kwa kumiliki kwa asilimia zaidi ya 60 na ushindi huo umewaweka katika nafasi nzuri ya kupenya kuingia robo fainali kutegemea na matokeo ya pambano la marudiano wiki mbili zijazo.
Pambano hilo litachezwa kwenye uwanja wenye rekodi nzuri kwa wenyeji kutofungika kirahisi wa Vicent Calderon mjini Madrid.

No comments:

Post a Comment