STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, February 18, 2015

Mourinho akiri sare ilikuwa kama zali kwa PSG

http://images.dailystar-uk.co.uk/dynamic/58/photos/879000/161879.jpg
Kipa aliyeibeba Chelsea jana ugenini dhidi ya PSG
MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amekiri kikosi cha kilikuwa na bahati kupata sare ya bao 1-1 katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya timu 16 bora dhidi ya Paris Saint-Germain. 
Katika mchezo huo Branislav Ivanovic ndiye aliyeifungia Chelsea bao la kuongoza kabla ya Edinson Cavani hajasawazisha. 
Akihojiwa mara baada ya mchezo huo, Mourinho amesema ukiona jinsi golikipa wake Thibaut Courtois alivyokuwa akiokoa michomo mingi ya wapinzani hakuna shaka kuwa ilikuwa bahati kwao kuibuka na ushindi. 
Mourinho amesema sasa karata iko upande wao kwani mchezo huo utaamuliwa katika Uwanja wa Stamford Bridge baada ya wiki mbili zijazo.

No comments:

Post a Comment