STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, February 18, 2015

Rooney aomba radhi kwa kujirusha

http://a2.fssta.com/content/dam/fsdigital/fscom/Soccer/images/2015/02/18/021815-Soccer-Manchester-United-Rooney-PI-CD.vadapt.620.high.0.jpgGOLIKIPA wa klabu ya Preston, Thorsten Stuckmann amesema Wayme Rooney alimuomba radhi kwa jinsi alivyodanganya na kupata penati katika mchezo wao dhidi ya Manchester United waliofungwa mabao 3-1. Rooney alianguka katika eneo la hatari baada ya kile kilichoonekana kama kuguswa na Stuckmann. Stuckmann alikaririwa na gazeti la The Sun akidai kuwa Rooney alimfuata na kumuomba radhi kwani ilikuwa nafasi yake ya kupata penati na alilazimika kuitumia.
Nyota huyo wa kimataifa wa Uingereza alifunga penati hiyo na kuihakikishia nafasi United ya kucheza hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la FA dhidi ya Arsenal.
Kitendo hicho cha Rooney kilizua mjadala mkubwa miongoni mwa wachambuzi wa soka lakini aliungwa mkono na kocha wa timu ya taifa ya nchi hiyo Roy Hodgson na mchezaji mwenzake wa zamani Phil Neville ambao walidai alijirusha ili kumkwepa golikipa.
Stuckmann mwenye umri wa miaka 33 amesema suala hilo liko wazi kuwa ile haikuwa penati lakini walipewa kwa sababu wenyewe ni United na kama ingekuwa mchezaji wao ndiye angefanya vile hadhani kama angepewa mkwaju huo.

Copy and WIN : http://bit.ly/copynwin

No comments:

Post a Comment