STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, May 10, 2015

Kibaka amliza Benni McCarthy, ampora kila kitu akiwa saluni

http://3.bp.blogspot.com/-YGgvai_tplY/Tv8nwIMi6YI/AAAAAAAAMrk/8yk4O-snDNU/s1600/32832.jpg

MSHAMBULIAJI wa zamani wa Afrika Kusini, Benni McCarthy ameporwa na mtu mwenye silaha wakati akiwa saluni ya kunyoa nywele jijini Johannesburg, Afrika Kusini. 
Wakala wa McCarthy, Percy Adams amesema mteja wake huyo alikumbwa na kadhia hiyo akiwa saluni hapo na kuporwa vitu vyake kadhaa vya thamani ikiwemo saa, hereni na pete yake ya ndoa. 
Adams aliendelea kudai kuwa katika tukio hilo hakuna aliyejeruhiwa na wateja wengine waliokuwemo hawakuguswa zaidi ya McCarthy peke yake. 
McCarthy mwenye umri wa miaka 37, amewahi kushinda taji la michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya akiwa na klabu ya FC Porto ya Ureno huku akishikilia rekodi ya kufunga mabao mengi katika timu yake ya taifa ya Bafana Bafana akiwa na mabao 32. 
Matukio ya uporaji wa kutumia sialaha yanaonekana kuwa ya kawaida nchini humo baada ya golikipa na nahodha wa Bafana Bafana kuuawa mwaka jana katika tukio kama hilo la uporaji akiwa nyumbani.

No comments:

Post a Comment