STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, May 10, 2015

Polisi Moro, Masau Bwire warudi Ligi Daraja la Kwanza

Mbeya City wamemaliza kwa ushindi nyumbani dhidi ya Polisi

Polisi wameenda na maji

Yanga walioendelea kutoa takrima kwa timu pinzani
 
Azam walimaliza kwa kishindo nyumbani

JKT Ruvu licha ya kichaapo cha Simba wamenusuurika kushuka draja

Ndanda wamepona baada ya kuilaza Yanga
Simba waliomaliza ligi kwa kishindo kwa kuiparua JKT Ruvu

Prisons wameponea chupuchupu
Mtibwa wamemaliza kwa kichapo nyumbani mbele ya Coastal Union
PAZIA la Ligi Kuu ya Tanzania Bara limehitimishwa kwa michezo saba na kushuhudiwa timu za Polisi Moro na Ruvu Shooting ya Msemaji mwenye tambo nyingi, Masau Bwire wakishuka daraja kwenda FDL.

Ruvu inayonolewa na kocha Mkenya Tom Olaba ilikuwa ugenini Uwanja wa Kambarage mkoani Shinyanga na kujikuta ikipokea kipigo cha bao 1-0 na wenyeji wao Stand United ambayo ushindi huo umeifanya kufikisha pointi 31 katika nafasi ya 10.

Polisi Moro iliyopanda kucheza Ligi Kuu msimu huu, ilikubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Mbeya City na kujikuta ikirudi ilipotoka na hiyo inatokana na mwenendo wa kusuasua tangu kuanza kwa msimu huu ikiwemo uongozi kubadilisha makocha mara kwa mara.

Polisi Moro ndiyo timu pekee msimu huu ambayo imefundishwa na makocha watatu, ilianza na Adolf Rishard 'Adolf' kisha ikamfukuza na kumchukua Amri Said, ambaye naye aliamua kujiondoa na nafasi yake kuchukuliwa na John Tamba, lakini hadi siku jana walijikuta wakiburuza mkia wakiwa na pointi zao 25 katika mechi 26 walizocheza.
Katika uwanja wa Nang'wanda Sijaona mkoani Mtwara, Mabingwa wapya wa msimu huu Yanga waliendelea kuonja shubiri baada ya kupoteza mchezo huo kwa kufungwa bao 1-0 na wenyeji Ndanda FC, Wakati kwenye Uwanja wa Azam Complex wenyeji Azam walitoka sare ya bila kufungana na Mgambo JKT ya Tanga.
Kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza kocha, Mbwana Makatta, alifanikiwa kuiokoa timu ya Tanzania Prisons isishuke daraja msimu huu baada ya kuilazimisha sare ya bila kufungana na Kagera Sugar aliyomaliza nafasi ya sita ikiwa na pointi 32, huku sare hiyo ikiwasaidia maafande hao kufikisha pointi 29 na kuepuka janga la kurudi kushuka daraja la kwanza msimu ujao.
Katika uwanja wa Manungu Turiani, Mtibwa Sugar ililala nyumbani kwa kufungwa mabao 2-1 na Coastal Union ya Tanga na matokeo hayo kuifanya timu hiyo iliyokuwa na kipindi kigumu licha ya kunza msimu huu vizuri kumaliza nafasi ya saba msimu huu ikiwa na pointi 31 huku Wagosi wa Kaya wakimaliza nafasi ya tano wakiwa na pointi 34.
Msimamo wa mwisho wa Ligi Kuu ya Bara:
                      P    W    D    L    F     A    Pts

1. Yanga         26  17    4    5    52   18   55
2. Azam         26   13   10   3    36   18   49

3. Simba        26   13    8    5    38   19   47
4.  Mbeya City26    8    10   8    22    22  34
5.  Coastal     26    8    10   8    21    25   34
6.Kagera        26    8     8   10   22    26   32
7. Mtibwa       26    7    10   9    25    25   31
8. JKT Ruvu    26    8    7    11   20    25   31
9. Ndanda      26    8    7    11    21   29   31
10.Stand        26    8    7    11    23   34   31
11. Prisons     26    5   14    7    18    22   29
12. Mgambo   26    8    5    13   18    28   29
13. Ruvu        26    7    8    11   16    29   29
14. Polisi Moro26    5   10   11   16    27   25

Matokeo:
JKT Ruvu       v  Simba            (1-2)
Mtibwa Sugar v  Coastal Union (1-2)
Stand Utd      v  Ruvu Shooting(1-0)
Mbeya City     v  Polisi Moro     (1-0)
Kagera Sugar v  Prisons          (0-0)
Ndanda          v  Yanga           (1-0)
Azam             v  Mgambo JKT  (0-0)

WAFUNGAJI:
17- Simon Msuva                                (Yanga)
14- Amissi Tambwe                             (Yanga)
11- Abaslim Chiidiebele               (Stand Utd)
10-Didier Kavumbagu                         (Azam)
     Rashid Mandawa              (Kagera Sugar)
     Emmanuel Okwi                             (Simba)
9- Malimi Busungu                         (Mgambo)
8- Samuel Kamuntu                      (JKT Ruvu)
    Ibrahim Ajibu                                  (Simba)
    Ame Ali                                         (Mtibwa)  
 7-Rama Salim                                   (Coastal)
6- Kipre Tchetche                                (Azam)
    Danny Mrwanda                             (Yanga)
    Heri Mohammed                             (Stand)
5- Jacob Massawe                           (Ndanda)
    Yahya Tumbo                                    (Ruvu)
    Atupele Green                               (Kagera)
    Mussa Mgosi                                (Mtibwa)
    Nassor Kapama                            (Ndanda)
4- Ally Shomari                                 (Mtibwa)
    Themi Felix                             (Mbeya City)
    Said Bahanuzi                        (Polisi Moro)
    Frank Domayo                                 (Azam)
    Mrisho Ngassa                                (Yanga)
    Kpah Sherman                                (Yanga)
    Gaudence Mwaikimba                   (Azam)
    Andrey Coutinho                           (Yanga)
    Ramadhani Singano                      (Simba)
3- Dan Sserunkuma                            (Simba)
    Elias Maguli                                     (Simba)
    Ally Nassor                                 (Mgambo)
    Raphael Alpha                       (Mbeya City)
    Aggrey Morris                                  (Azam)
    Paul Nonga                             (Mbeya City) 

NB:WAKILISHI WA NCHI, ZILIZOSHUKA DARAJA

No comments:

Post a Comment