STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, May 10, 2015

Rais TFF awapo pole wahanga wa mafuriko

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/04/malinzi11.jpg
Rais wa TFF, Jamal Malinzi
Na Rahma White
RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ametuma salamu za pole kwa wakazi wa Dar es salaam na hasa wale walioathirika na mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar es salaam kwa siku ya tatu mfululizo sasa.
Katika salamu zake kupitia kwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam, Mecky Sadik, Malinzi amesema familia zimepoteza makazi, miundombinu ya usafiri na michezo imeharibika na hata kuwa katika hali ya kutotumika, wanawake watoto, familia, shughuli za kiuchumi na kimichezo zimeathirika na mvua hizi.
TFF inaunga mkono juhudi za Mkuu wa Mkoa Dar es salaam, Serikali na wadau wote wanaoshugulika  kupunguza makali ya janga hili.

No comments:

Post a Comment