STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, May 10, 2015

Ngumi kupigwa mjini Bagamoyo, Super D kugawa vifaa kwa wakali

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiQeWrEKx0_mnCSl1J8PJPUA6_zw9p_yAOeZomH3PlujJqmd-14VYhlB3pKSf7PHU9eX1DZtKUMI9cS9-QGU2VjQhu79Pbzw72lNYISSHPE4Pp4xjpa8cUno_Tb72KVlAzOr64GIftMRVk/s1600/10702151_751229401589872_1190688698899816254_n.jpg
Super D akionyesha baadhi ya DVD anazosambaza kwa ajili ya kutoa mafunzo ya ngumi,
Na Rahim Kimwaga
NDONGA zinatarajiwa kupigwa mjini Bagamoyo wakati mabondia Idd Pialali wa Kiwangwa atakapopanda ulingoni kuzipiga na Adam Ngange wa Chanika katika pambano liotakalochezwa Mei 16.
Mpambano huo utapigwa kwenye ukumbi wa Che kwa Che, uliopo mjini humo na tyari kila bondia ameanza tambo akijigamba kuibuka na ushindi siku hiyo.
Mbali na pambano hilo lililoandaliwa na kampuni ya Sharrif Promotion, pia siku hiyo kutakuwa na mapambano mengine kadhaa ya utangulizi yatakayowahusisha mabondia machachari.
Kwa mujibu wa mratibu huyo mabondia watakaowasindikiza Pialali na Ngange ni pamoja na lile litakalowakutanisha Rashidi Haruna dhidi ya Kaminja Ramadhani.
Michezo mingine ni kati ya Halid Hongo atakayebiliana na Kishoki Mbish, huku Abdallah Samata atazidunda na Maono Alli 
Mgeni rasmi katika pambano hilo ambalo viiongilio vyake vinaanzia Sh. 5000 kwa viti vya kawaida na Sh. 8000 kwa V.I.P atakuwa ni bodnia Cosmas Cheka, mdogo wa bingwa wa zamani wa dunia wa WBF, Francis Cheka 'SMG'.
Pia katika mipambano hilo, kutakuwa na upatikanaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi  kali pamoja na kutambua sheria zake zikiwa na mabondia wakali kama vile
Floyd Mayweathar vs Manny Paquaio 2015 , Saul 'canelo' Alverez, Mike 'Iron' Tyson, Muhammad Ali, Felix Trinidad, Miguel Cotto na wengine wengi, huku vifaa vya mchezo vitagawiwa na kocha  Rajabu Mhamila 'Super D' kwa mabondia watakaofanya vizuri siku hiyo na vingine vitauzwa kwa gharama nafuu na kocha huyo kwa ajili ya kuamasisha mchezo wa masumbwi nchini.

No comments:

Post a Comment