STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 12, 2015

Lisome Tamko la Viongozi wa Wanachuo wa KIU

Wanachuo wa KIU Tanzania wakiwa katika maandamano hayo ya hivi karibuni


WANAFUNZI WA KITIVO CHA SAYANSI YA TIBA CHUO KIKUU CHA KIMATAIFA CHA KAMPALA, GONGO LA MBOTO DAR ES SALAAM

Kutokana   na matatizo mbalimbali ya chuo kikuu kishiriki cha Kampala, ambayo yamesababisha kuwa na migomo ya mara kwa mara katika kitivo cha afya. Na yamefikishwa katika ngazi mbalimbali za uongozi wa serikali ikiwemo wizara ya Elimu, wizara ya Afya na Bunge.
   
        MATATIZO:
Chuo chetu kinakabiliwa na matatizo mengi ambayo kwa namna moja au nyingine yanarudisha nyuma maendeleo ya wanafunzi kimasomo, matatizo hayo ni kama ifuatavyo;
1.      Kutokusajiliwa kwa kada zote za afya katika bodi husika za afya nchini ( ambazo zinatolewa chuoni hapa.
Kada ya udaktari, ufamasia na maabara hazina usajili wa bodi husika zinazosimamia taaluma hizo zikiwemo pharmacy council, Tanganyika medical association na medical laboratory council na NACTE (kwa wanafunzi wa diploma na certificate). Kutosajiliwa kwa kada hizo kunapelekea wanafunzi wanaohitimu chuoni hapo kutotambulika hivyo kupelekea kukosa ajira.
2.      Kusimamishwa masomo kwa wanafunzi 5 bila sababu za msingi na kupewa kesi ambazo    hawajasifanya
3.      Kiwango kikubwa cha ada(tuition fee)
Kikao cha tarehe 13/11/2014 kilichofanyika wizara ya elimu kilitoa mapendekezo ya kupunguza ada kwa chuo cha kampala lakini hakuna utekelezaji mpaka sasa. Kwa mfano kwa mwaka wa masomo 2013/2014 wanafunzi wa kada ya ufamasia wa ngazi ya shahada wanalipa tsh 5,400,000/=. Wakati wale wa mwaka wa masomo 2014/2015 wanalipa ada kiasi cha tsh 3,800,000/=. Kwa wanafunzi wa kada ya udaktari ngazi ya shahada mwaka wa masomo 2013/2014 wanalipa tsh 9,900,000/=. Wakati wa mwaka wa masomo 2014/2015 wanalipa kiasi cha tsh 6,700,000/=. Kwa wanafunzi wa stashahada ya udaktari,famasi na maabara wanalipa kiasi cha tsh 1,900,000/=.
4.      Mtaala wa kufundishia(curriculum).
Chuo chetu kinatumia mtaala tofauti na ule wa Tanzania(wa Uganda) ambao unawapa ugumu baraza husika kukisajili chuo chetu. Mtaala huo pia unawapa kazi sana wanafunzi katika kufuatilia na kuyaelewa yale wanayofundishwa kwan umebeba masomo mengi kwa muhula mmoja kwa mfano wanafunzi wa shahada ya ufamasia wanasoma masomo 11 kwa muhula mmoja katika chuo chetu wakati ni tofauti ukilinganisha na vyuo vingine ambavyo kwa muhula mmoja wanasoma masomo 4 hadi 5. Kwa wanafunzi wa stashahada wanasoma hadi masomo 15 kwa muhula mmoja ambayo kwa hali ya kawaida huwezi kuyamudu kwa wakati.
5.      Utaratibu wa supplementary.
Supplementary zinafanyika kila baada ya muhula wa masomo na kwa kila somo mwanafunzi anawajibika kulipia tsh 40,000/= wakati ukilinganisha na vyuo vingine supplementary zinafanyika mwisho wa mwaka wa masomo na mwanafunzi halipii kabisa au kuchanga kiasi kidogo sana kwa ajili ya mitihani hiyo. Pia mwanafunzi anawajibika kurudia muhula endapo atafeli mtihani wake wa supplementary hata kama ni somo moja tu na atalazimika kurudia masomo yote hata yale ambayo alifaulu vizuri.


6.      Uongozi mbovu wa kitivo cha sayansi ya afya(health science).
Uongozi wetu hauna mfumo unaoeleweka wa utoaji matokeo ambapo katika mtihani mmoja mwanafunzi anapokea matokeo yake mara tatu tofauti. Kutokuonekana kabisa kwa matokeo ya baadhi ya wanafunzi hii inachangiwa pia na mfumo wa utoaji matokeo hayo ambapo mpaka leo hii wanafunzi wa chuo wanabandikiwa matokeo ubaoni kama wanafunzi wa shule ya msingi. Pia uongozi hauna mazoea wala utaratibu wa kumsikiliza mwanafunzi.
7.      Uhaba wa miundombinu ya chuo.
Chuo chetu kinakabiliwa na uhaba mkubwa wa vifaa vya ufundishaji na ujifunzaji hasa maabara, vingine ni kama projector na microphone ambapo utakuta darasa la watu zaidi ya 100 halina microphone na kuoelekea baadhi ya wanafunzi kuhudhuria darasani bila kupata chochote kutokana na kutokumsikia kabisa mwalimu. Pia Chuo hakina usafiri wa uhakika kwa ajili ya medical rotation na research mbalimbali.
8.      Ada ya TCU.
Chuo chetu kina utaratibu wa kuwaibia wanafunzi wa stashahada na astashahada kwa kuwalipisha kiasi cha tsh 20,000/= kama ada ya usajili wa TCU wakati TCU wala hawahusiki na wanafunzi hao.huu ni wizi wa dhahiri kwani hizo fedha wanalipa kupitia account ya chuo na sio TCU.
9.      Ukosefu wa uwiano kati ya wafanyakazi wa chuo.
95% ya wafanyakazi wa chuo chetu ni wageni na sio watanzania hivyo kupelekea hata matatizo yetu kutopata suluhu na uangalizi wa karibu kwani wengi wa wafanyakazi hao hawajali hali halisi ya watanzania.
10.  Pesa maalumu kwa ajili ya kada mbalimbali(special faculty requirement).
Kutokana na majibu yaliyotolewa katika kikao kilichofanyika tarehe 04/05/2015 kati ya uongozi wa chuo na bodi ya mikopo ya elimu ya juu(HESLB) imeelezwa kwamba chuo chetu kinakosa fedha hizo kutokana na kukosa usajili wa kudumu.
11.  Masomo ya pre entry(MPP)
Chuo chetu kina utaratibu mbovu wa kuwafundisha masomo ya sekondari wanafunzi wa shahada wanaochaguliwa chuoni hapa na masomo hayo hufundishwa kwa muhula mzima na kupelekea kuongezeka muda wa kuhitimu masomo yao huku wakilipa ada ile ile. Hai hii hupelekea wanafunzi kuwa na muda mfupi wa likizo kwa ajili ya recessive semester ambayo wanafidia muda waliosoma masomo ya sekondari(MPP) badala ya course husika.
12.  Muda wa kuhitimu masomo``
Wanafunzi wa shahada wameongezewa muda wa kukaa chuoni hii ni kutokana na urasimu wa chuo na uwepo wa masomo ya pre entry au MPP ambapo mwanafunzi wa kada ya maabara anatakiwa kusoma kwa miaka 4.5 badala ya miaka 3 na kada za udaktari na ufamasia wameongezewa miezi 6 ambapo madaktari wanasoma miaka 5.5 badala ya miaka 5 na wafamasia wanasoma miaka 4.5 badala ya miaka 4 kitu ambacho ni kinyume kabisa na utaratibu wa elimu ya Tanzania.
13.  BRIDGING COURSE NA UDAHILI WA WANAFUNZI KINYUME NA UTARATIBU.
Kumekua na udahili wa moja kwa moja wa wanafunzi wasio kua na vigezo katika chuo hiki kinyume na utaratibu,wakifundishwa masomo ya bridging course ambayo ni kinyume cha sheria,ambayo pia haipo chuo chochote Tanzania na ilikua ni moja ya sababu zilizo pelekea chuo cha tiba cha IMTU mwaka 2014 kufungiwa.  Je,serikali inakiwajibisha vipi chuo hiki ambacho kinakwenda kinyume na taratibu hizo pamoja na wanafunzi ambao wizara imethibitisha mbele ya waziri kua haitawasajili,chuo kinawafidia vipi wanafunzi hao?
14.  Ukosefu wa prospectus na university calendar,
Chuo hakina prospectus wala university calendar  inayowaongoza wanafunzi na wafanyakazi kwa ujumla na kuwaonyesha ratiba na  matukio ya mwaka mzima.
15.  Kudahiliwa katika chuo cha nje ya nchi wakati tumeomba kama wanafunzi wa ndani ya nchi na tunapata mkopo tukitambulika kama wanafunzi wa ndani ya nchi, hii inatuletea shida ya kutambulika kama wanafunzi wa kigeni na kutakiwa ku verify vyeti vyetu kabla ya kuajiriwa nchini kwetu tofauti na vyuo vingine vilivyopo nchini  ambavyo vipo chini ya TCU.

 MAJIBU YA WAZIRI WA ELIMU MUHESHIMIWA SHUKURU KAWAMBWA
Baada ya wanafunzi wa kitivo cha sayansi ya tiba katika chuo kikuu kishiriki cha Kampala kukumbwa na matatizo mbalilmbali ambayo yameshindwa kutatuliwa katika ngazi mbalilmbali mpaka pale yalipofikishwa katika bunge la jamuhuri ya muungano wa Tanzania na kuundwa kamati ili kuweza kushugulikiwa  matatizo hayo .
 kamati ilipewa muda wa wiki moja kuweza kukamilishwa kwa kazi hiyo tarehe 4 mwezi huu wa sita  leo  hii ni wiki moja imepita na kamati hii haijafika.
Lakini cha kushangaza tulipata ugeni jana tarehe 10/06/2015 Mh Shukuru Kawambwa waziri wa elimu nchini ambapo alipanga kuonana na uongozi wa chuo pamoja na serikali ya wanafunzi bila kuwaona wanafunzi wenye matatizo husika, ambapo baada ya wanafunzi hao kugundua walimuomba waweze kuongea nae kuhusu matatizo hayo ambayo yameshindwa kupatiwa ufumbuzi kwa miaka mingi sasa  na muda huo wanafunzi wote wa kitivo cha sayansi ya afya chuoni hapa tulisimamishwa masomo kwa siku zisizojulikana kuanzia tarehe 8/06/2015.Na muheshimiwa waziri alipanga kujibu matatizo ya chuo hicho yasiyopungua 15 kwa muda wa dakika 30 akiwa anadai kwamba anawai ndege kwa ajili ya safari ya saa 12 jioni.
N.B: kuja kwa waziri hakujatatua tatizo lolote bali kumeongeza matatizo kwa sababu tarehe 1/06/2015 alikiri mbele ya bunge kuwa matatizo ya chuo kikuu cha kampala hayawezi kutatuliwa na serikali yake.
       MAJIBU YA WAZIRI KUHUSU MATATIZO HAYO.
1;KUHUSU USAJILI
Waziri alikili wazi kwamba chuo kimesajiliwa kama chuo cha nje na Tume ya vyuo vikuu Tanzania(T.C.U) Na kudai kwamba vyuo kama hivyo nchini vipo ambapo alipata kutolea mfano wa vyuo kama vile Jommo Kenyata university,Aga khan university bila kujali kwamba vyuo hivyo havipo katika orodha ya vyuo vinavyotambulika na Tume ya vyuo vikuu nchini Tanzania(T.C.U) .
     Hoja za Wanafunzi katika hili jibu ni kama ifuatavyo.
Sisi kama Watanzania halali wa nchi yetu tunashangazwa na majibu hayo maana sisi tumeomba kama wanafunzi wa ndani katika vyuo vitano tulivyopaswa kuomba na kupangiwa masomo hayo na Tume ya vyuo vikuu Tanzania katika chuo hiki cha Kampala international university  ambacho hakifuati kanuni na taratibu za nchi yetu ya Tanzania.
        Lakini hoja iliyokuwa kubwa zaidi hiki kama ni chuo kilichopata usajili kama chuo cha nje ni kwa nini basi wanafunzi tunapata mikopo ya serikali kama vyuo vya ndani wakati hii ni kinyume maana mikopo hutolewa kwa wanafunzi wa ndani tuu na isiwe scholarship kama ilivyo kwa wale wanaosoma nje za nchi.Ambapo hata hivyo vyuo alivyotolea mfano mheshimiwa waziri havitambuliki na tume ya vyuo vikuu nchini (T.C.U) pamoja na bodi ya mikopo ya Elimu ya juu nchini(H.E.S.L.B)
           Hata hivyo elimu inayotolewa katika chuo hiki cha kimataifa hakiendani na vyuo vingine vya kimataifa na hata vya ndani na sisi wanafunzi wa chuo hiki imepelekea kudharaulika na kuwa na uwasiwasi na soko la ajira hapo baadae endapo tutamaliza salama katika chuo hiki ambacho wanafunzi wadai haki tena kwa njia ya amani hunyanyaswa kwa kusimamishwa masomo ,kupelekwa lumande na kusingiziwa kesi mbalimbali ili waweze kukwamishwa katika masomo yao.
     2; MITAALA YA CHUO HIKI.
Majibu ya waziri huyo mwenye dhamana ya elimu nchini yameonesha wazi kwamba mitaala hiyo imepitishwa na jopo wataalam  maprofesor wengi kutoka chuo kikuu cha Dar es salaam(U.D.S.M) na kupitishwa na tume ya vyuo vikuu nchini(T.C.U)
  Na mheshimiwa waziri alipata kuongeza wazi kwa kusema kwamba bodi za afya yaani ile ya famasia,mahabara na udaktari haziusiki na mambo ya mitaala bali ni T.C.U peke yake ndio inahusika.
     Hoja za wanafunzi kuhusu jibu hili
Sote tunajua wazi kwamba chuo kikuu cha Dar es salaam hakina kozi za afya sasa bado tunakosa  imani na waziri maana haiwezekani mitaala hii kutungwa na watu wenye fani tofauti na zile za afya hata wawe maprofesor gani maana hii kazi inabeba maisha ya watu hivyo basi tunaomba bodi husika kupitisha mtaala huu.
Pia tukirejea barua kutoka baraza la famasia iliyotumwa katika chuo hiki yenye Kumbukumbu namba  AB/300/312/02/20,ya tarehe 14/04/2015 inaeleza moja ya matatizo ambayo yanafanya chuo hiki kutosajiliwa ni pamoja na mtaala unaotumika ambao ni kinyume na mtaala wa Tanzania  ulioanzishwa kwa mujibu wa sheria  ya famasia Cap 311 na pia chuo hiki kilikumbushwa na TCU suala hili kwa barua yenye kumbukumbu namba TCU/A.40/1/VOL.II/14 ya tarehe 16/12/2014 na hata tarehe 4/6/2015 mbele ya bunge waziri wa afya alisema wazi kwamba hawawezi kumsajili mwanafunzi yeyote kama mtaala wa chuo chake haujapitishwa na bodi husika na taaluma inayotolewa na chuo husika iwe inakubalika.
     
Matatizo haya tumeweza kuyapitisha katika ngazi mbalimbali za kiserikali ikiwemo Tume ya vyuo vikuu nchini,bodi husika,kwa mkuu wa wilaya ya ilala na huko kote hatukupata ufumbuzi wa matatizo haya mpaka sasa tupo ngazi ya bunge.
          Hivyo basi sisi wanafunzi wote wa kitivo cha sayansi ya tiba katika chuo cha kimataifa kampala tunakiri wazi kwamba hatuna imani na majibu ya waziri wa elimu mh.Shukuru Kawambwa


HOJA ZA WANAFUNZI WOTE KWA UJUMLA WA KITIVO CHA SAYANSI NA TIBA
1.Uhalali wa hotuba wanazotoa hawa viongozi zinazopingana kama zile zinazotolewa na waziri wa elimu pamoja na waziri wa afya mwenye dhamana husika.
2.Kuto kuwepo kwa kwa uthibitisho sahihi wa juu ya usajili wa kozi husika katika  bodi zake.
3.Matumizi ya nguvu katika kutatua  mambo ya wazi kabisa ambayo ni muhimu kama vile matumizi ya mabomu ya machozi na maji ya kuwasha kwa siku ya tarehe 8/06/2015
4.Bodi ya mikopo inatoaje mikopo katika chuo kilichosajiliwa kama chuo cha nje
5. Kwanini serikali inaruhusu chuo cha kimataifa Kampala (K.I.U) kisisimamiwe na  BODI ZA UFAMASIA ,MAHABARA ,na UDAKTARI zenye lengo la kusimamia ubora wa taaluma  ikiwa pamoja na kusimamia mitaala na kudhibiti  viwango vya waalimu wenye sifa  kufundisha  kozi za afya nchini kuliko ilivyo hivi sasa  ambapo mitaala haitambuliki na bodi hizo husika.
       
 
SISI KAMA  WANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA KAMPALA TUNALAANI  VIKALI MATENDO                                      YAFUATAYO  TULIYOFANYIWA KATIKA VIPINDI HIVI VYA MGOMO MPAKA SASA

1.Wanafunzi kufukuzwa chuo kila wanapodai haki zao ambapo siku ya tarehe 30/04/2015 jumla ya wanafunzi kumi na sita ambao baadhi yao walikuwa wana kamati ya kufuatilia matatizo haya walisimamishwa masomo .na tarehe 2/06/2015 jumla ya wanafunzi watano walisimamishwa masomo kwa madai hayohayo na wanafunzi wapatao takribani 19 walipata kulala mahabusu kwa makosa yasiyoeleweka.
    
 2.polisi kutumia nguvu kutawanya wanafunzi ambao wamekaa na hawafanyi vurugu zozote na waliotii amri za kipolisi kwa kukaa chini hii tumeona siku ya tarehe 8/06/2015 ambapo polisi waliwamwagia wanafunzi maji ya kuwasha na kupiga mabomu na kuleta uvunjifu wa amani ambapo walisababisha wanafunzi wengi waliumia na wengine bado wapo katika matibabu mpaka sasa,masomo kusitishwa kwa wanafunzi wa shule za msingi zilizo karibu na chuo kutokana na ulipukaji wa mabomu ya machozi vilevile kuathirika kwa wagonjwa katika kituo cha afya cha gongo la mboto kilicho jirani na chuo.

3.Viongozi mbalimbali wa kiserikali kuacha matatizo haya mpaka yanafikia hali hii kwamba wanafunzi wanahitimu taaluma yao na kushindwa kuajiliwa.

4.Tunalaani vikali uongozi wa chuo hiki kwa kushindwa kufuatilia  haya mapaka yanafika hatua hii.

                                                           
                MATATIZO AMBAYO HAYAJAFANYIWA UFUMBUZI HADI SASA

                                                                                        
                               
1.      Mitaala(curriculum) haijarekebishwa ili ifanane na vyuo vingine. Ref. TCU reg no. 40 ibara A uk. 17, reg no. 47 uk. 20 na reg no. 62 uk. 25
2.      Kukosekana kwa kalenda inayomuongoza mwanafunzi kwa mwaka mzima na kumuonesha utaratibu na ratiba za chuo mpaka sasa.
3.      Waalimu wengi wao kuto kuwa na sifa ya kufundisha kozi husika. Ref TCU reg no. 14 ibara ya 4.
4.      Kukosekana kwa uwiano sawa kati ya wafanyakazi wazawa na wageni hasa kwa ngazi za juu. Refer TCU Reg no. 14 ibara ya 3.
5.      Masomo ya pre entry ama MPP hayajatolewa  kabisa hasa ikizingatiwa masomo haya huchukua semester mzima na kuchelewesha wanafunzi kuendelea na kozi zao husika.
6.      Muda wa kuhitimu masomo uwe sawa na vyuo vingine kama utaratibu wa elimu ya nchi unavyotambua.
7.      Kusajiliwa kwa kada za sayansi ya afya na tiba katika bodi husika(full registration).
8.      Uongozi wetu haujabadilishwa akiwemo dean of faculty of health and applied science.
9.      Ada haujashuka  kama utaratibu wa TCU na wizara ya elimu ulivyoelekeza.
10.  Wanafunzi  wote waliosimamishwa  hawajarudishwa  maana walipewa kesi nyingi za kusingiziwa  na  zisizoeleweka



     MSIMAMO WA WANAFUNZI:
Kutokana na matatizo tajwa hapo juu ambayo yamekuwa na mizozo mikubwa sana hapa chuoni sisi kama umoja wa wanafunzi wa kada za afya tuna misimamo ifuatayo.
·         Bado tunaiomba serikali ituhamishe sehemu hii maana si salama kwetu sisi wanafunzi na haina uhakika wa kozi zake hali inayofanya wanafunzi weng huacha masomo.
·         Hatupo tayari kurudi katika majengo ya kampala international university mpaka matatizo yetu yapatiwe ufumbuzi(Tuhamishwe) ili chuo hiki kimalize matatizo hayo tajwa  maana ni mwaka mzima umekwisha bila sisi kusoma masomo yaliyopo kwenye kozi za afya


MASWALI YA MSINGI KWA WIZARA HUSIKA
1.      Kwanini wizara ya elimu idahili wanafunzi kuja kusoma kampala int. university bila kuwasiliana na wizara ya afya na bodi husika?.
2.      Kwanini chuo kinachukua wanafunzi wasiokuwa na vigezo kwa direct entry?
3.      Nini hatima ya waathirika wa matatizo haya ambao wamemaliza chuo na wamekosa ajira na kwa wale wanaoendelea?
4.      Ni hatua zipi za kisheria zinachukuliwa juu ya chuo hiki ikiwa chuo cha IMTU kilikuwa na matatizo machache kuliko haya lakini kilifungiwa?
              NB:Tamko hili limetolewa na Mwenyekiti  Mteule wa Wanafunzi, David Payovela na Katibu wake Jackson Raymond.

No comments:

Post a Comment