STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 12, 2015

Nani kasema eti Messi na Ronaldo ni mahasimu?!

MSIKIE Leonel Messi anavyosema baada ya kuzuka kwa taarifa kwamba ni hasimu mkubwa na Cristiano Ronaldo. Mshambuliaji huyo nyota wa Barcelona na Argentina, amesisitiza kuwa hana uhasama wowote na nyota wa Real Madrid Cristiano Ronaldo. Wawili hao wanahesabiwa kama wachezaji bora kabisa duniani kwasasa wakiwa wameshinda tuzo saba za Ballon d’Or zilizopita kati yao. Ronaldo ambaye ndio alionyakuwa tuzo mbili za mwisho na kuwafanya wadau wa soka kudai kuwa mafanikio ya nyota huyo wa kimataifa wa Ureno ndio yaliyomhamasisha Messi naye kucheza kwa kiwango cha juu msimu huu. 
Hata hivyo, Messi amesisitiza kuwa haathiriki na kitu chochote ambacho Ronaldo anakifanya ndani na nje ya uwanja. 
Messi amesema hakuna wala hakujawahi tokea uhasama wowote kati yao kwani jambo hilo limetengenezwa na vyombo vya habari zaidi kuliko uhalisia na kusisitiza kila mtu anajisikia vema kwa mwenzake.

No comments:

Post a Comment