STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 12, 2015

Liverpool Jeuri! Yaigomea Man City kwa Raheem Sterling

KLABU ya Liverpool jeuri sana! Imeamua kuikataa ofa ya Pauni Milioni 25 iliyotolewa na klabu ya Manchester City inayomtaka mshambuliaji wake Raheem Sterling. Liverpool wanamthaminisha nyota huyo wa Kimataifa wa England ambaye pia anahusisha na tetesi za kutakiwa Arsenal na Real Madrid, kufikia Pauni Milioni 50. Sterling mwenye umri wa miaka 20 alijiunga na Liverpool akitokea Queens Park Rangers mwaka 2010 na yuko chini ya mkataba mpaka mwaka 2017. Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers alisema mwezi uliopita kuwa anamtegemea nyota huyo kubakia Anfield mpaka mkataba wake utakapokwisha baada ua kukataa kusaini mkataba mpya ambao ungemuwezesha kulipwa kitita cha Paundi 100,000 kwa wiki.

No comments:

Post a Comment