STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 12, 2017

Wenger kumbe hata huyu naye ulimkosa?

KOCHA Arsene Wenger amekuwa akihusishwa na kushindwa kunyakua nyota mbalimbali kutokana na kuwa mgumu kutoa fedha zinazohitajiwa na klabu husika. Orodha hiyo kwa sasa imeangukia kwa beki wa AS Roma. Wakala wa beki huyo Kostas Manolas amedai kuwa AS Roma ilikataa kitita cha euro milioni 40 kutoka Arsenal ili kumnasa nyota huyo msimu huu.
Arsenal walikuwa wakihusishwa na usajili wa beki huyo katika kipindi cha usajili wa kiangazi mwaka jana, lakini suala lake halikufanikiwa baada ya kumchukua Shkodran Mustafi kutoka Valencia badala yake. Wakala wa beki huyo amesisitiza kuwa kiasi cha fedha walichokitaka Roma ndio kilikuwa chanzo kikubwa cha kuvurugika kwa dili hilo. Hata hivyo wakala huyo aliendelea kudai kuwa Kostas anaweza kuondoka Juni mwaka huu ingawa ameondoa uwezekano wa kwenda China.

No comments:

Post a Comment