STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 12, 2017

Schneiderlin huyooo Everton, Man United yakubali kumuuza

HAKUNA namna tena. Klabu ya Manchester United imekubali kumuuza kiungo wake Morgan Schneiderlin kwenda Everton kwa kitita cha pauni milioni 22. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye umri wa maiak 27, alisajiliwa United na Louis van Gaal kwa kitita cha pauni milioni 25 akitokea Southampton Julai mwaka 2015. Toka atue United amecheza mechi 47, lakini msimu huu amefanikiwa kucheza mechi nane pekee chini ya Kocha Jose Mourinho zikiwemo mechi tatu za Ligi Kuu.
Kwa upande mwingine Everton imekubali kumpeleka kwa mkopo mshambuliaji Oumar Niasse mwenye umri wa miaka 26 kwenda Hull City. Nyota huyo wa kimataifa wa Senegal alisajiliwa kwa kitita cha pauni milioni 13.5 kutoka Lokomotiv Moscow Februari mwaka jana, lakini hajafanikiwa kung’ara baada ya kucheza mechi saba pekee.

No comments:

Post a Comment