STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 12, 2017

Liverpool majanga, yapigwa kidude na Southampton

Nathan Redmond akishangilia bao lake alililowatungua Liverpool usiku wa jana kwenyer Uwanja wa St Mary's katika mechi ya nusu fainali ya Kombe la Ligi (EFL)
LIVERPOOL imekwama aisee, baada ya usiku wa kuamkia leo kuchapwa bao 1-0 na Southampton katika mechi ya Nusu Fainali ya kwazna Kombe la Ligi.
Kwa ushindi huo, Southampton imejiweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele kama itafanya kweli kwenye mechi ya marudiano ugenini Januari 25.
Bao lililowazamisha vijana wa Jurgen Klopp liliekwa kimiani na Nathan Redmond katika dakika ya 20 katika mchezo huo mkali uliopigwa kwenye Uwanja wa St. Mary's mjini Southampton.
Kipigo hicho cha Liverpool kimekuja siku chache tangu walipong;anganiwa na timu ya daraja la chini ya Plymouth katika mechi tya raundi ya tatu ya Kombe la FA ambao watarudiana nao Januari 18.
Wikiendi hii Liverpool itakuwa na kibarua kigumu mbele ya Man United ambayo juzi iklipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Hull City katika mechi ya kwanza ya nusu fainali ya Kombe la Ligi na kujiweka pazuri kutinga fainali.
Vijana wa Klopp watakuwa na wiki ngumu kwa kutakiwa kucheza mfululizo mara baada ya kuumana na Man United Jumapili hii.

No comments:

Post a Comment