STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 12, 2017

Zaha aanza mambo Ivory Coast ikiilipua Uganda x3

Straika Serge Aurier akishangilia bao la tatu la Tembo ya Afrika dhidi ya Uganda The Cranes
STRAIKA Wilfried Zaha akiichezea Ivory Coast kwa mara ya pili tangu alipoikana England, ameanza kuonyesha cheche zake baada ya kufunga bao lake la kwanza kwa Tembo hao wa Afrika wakiichapa Uganda kwa mabao 3-0.
Pambano hilo lilikuwa la kirafiki la kimataifa kujiandaa na michuano ya Afcon 2017 inayoanza wikiendi hii na lilichezwa nchini Ivory Coast na kushuhudia mpaka mapumziko hakuna timu iliyoona lango la mwenzake.
Zaha anayeichezea Crystal Palace wa England,  alifunga hilo katika dakika ya 58, ikiwa ni la pili kwa timu yake kwani dakika saba nyuma yake Jonathan Kodjia kuifungia Ivory Coast bao la kwanza.
Bao jingine la Serge Aurier katika dakika ya 72 na kuwazamisha wawakilishi wa ukanda wa Cecafa, Uganda ambayo inaends Gabon ikiwa ni mara ya kwanza tangu miaka 38 iliyopita waliposhiriki fainali hizo za Afrika.
Katika mechi nyingine ya kimataifa za kirafiki kwa maandalizi ya Afcon 2017 itakayochezwa Gabon kuanzia wikiendi hii, Senegal iliitambia Congo kwa mabao 2-0.

No comments:

Post a Comment